06/04/2026
SOMO: TELEVISHENI NA UMIZIMU
π Moja ya maendeleo makubwa ya teknolojia yaliyoshuhudiwa katika karne iliyopita ni uvumbuzi wa televisheni.
Ilipokuwa ikiingia duniani, iliidhinishwa kwa ajili ya mafunisho ya maadili kwamba ingezielimisha jamii.
π Hata hivyo, nashangaa mmomonyoko wa maadili leo unachangiwa zaidi na hizi televisheni.
Kwa sasa televisheni zimeanzishwa sana kiasi kwamba katika kila nyumba iliyo na heshima na utaratibu mzuri zinapatikana.
π Kwa sasa, zimefanywa kuwa ni hitaji la muhimu kwa kiwango kikubwa.
Ni ngumu katika akili ya yeyote kukataa kwamba maovu mengi yanayosababishwa na hizi skrini tofauti na kuchangia katika maadili mema k**a ilivyodaiwa kwamba ndio makusudi yake.
π Miongoni mwa mambo hayo ni picha za nusu uchi, uharifu na udanganyifu mara nyingi huonyeshwa katika sinema mbalimbali na matangazo.
Moja ya mambo ya hatari katika televisheni ni uovu ambao unapandikizwa katika akili na maisha ya mamilioni ya watu, nao ni UMIZIMU.
*Ninimaanaya UMIZIMU?*
π Mzizi wa *UMIZIMU* tunaweza kuupata kwa kutazama katika mianzo ya wakati, ambapo malaika aliyeanguka akiwa amejificha katika umbo la nyoka alipotamka maneno yake ya kwanza ya kilaghai kwa mwanadamu;
_"Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa... kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa k**a Mungu, mkijua mema na mabaya_." *(Mwanzo 3:4-5)*.
π _Mungu alikuwa ameshawaambia wanadamu kuwa endapo wangekula matunda ya mti uliokatazwa, wangekufa hakika_ *(Mwanzo 2:16,17)*.
π Shetani alisema kwamba hawatakufa (akimaanisha kwamba wana roho zisizokufa) bali pia kwamba wangekuwa k**a Mungu.
π Umizimu umejengwa katika msingi wa kanuni hizi mbili:
1. *Roho kutokufa na kwamba mtu anapokufa anakua mungu*.
2. *Kupitia msingi huu, shetani amefanya njia ambapo mtu anaweza kuwasiliana na mapepo*.
π Biblia iko wazi, kwamba wafu hawajui neno lolote *(Mhubiri 9:5)*.
π Shetani hufundisha kwamba mwili hufa bali roho haifi.
βοΈ _"Umizimu hufundisha kuwa hapana kifo wala dhambi wala hukumu wala adhabu; kwamba wanadamu ni nusu miungu ambao hawakuanguka dhambini; kwamba tumaini ndilo kanuni kuu; na kwamba mwanadamu huwajibika kwa ajili yake mwenyewe_." *(E.G. White: Patriarchs and Prophets, 688.1)*.
*Historia ya Imani za Umizimu*
π Tangu nyakati za zamani, wanadamu walikuwa wakifundishwa kuwa wafu huenda kwenye jua, mwezi au wamekuwa miongoni mwa nyota au sayari.
π Katika baadhi ya jamii kuna imani kwamba roho za wafu huingia kwa baadhi ya wanyama; na wengine huamini kuwa wafu hufanya sehemu katika kupatanisha wanadamu kwa Mungu, kwa mfano roho za mababu.
π Shetani alitambua kuwa endapo angewafanya wanadamu waamini mambo hayo, hivyo angeweza kuwafanya waabudu sanamu.
π Tunasoma kuhusu ibada kwa jua, ibada kwa ngβombe jike na dume, ibada kwa Mungu kupitia mababu;
Tunasoma kuhusu njia za mawasiliano na mapepo, uchawi β wale wanaodai kuwa na mawasiliano na roho za wafu.
π Tukiwatunatambua kuwa wafu hawajui lolote, bila shaka ni wazi kuwa watu hawa hawawasiliani na roho zilizokufa bali na malaika walioanguka β mapepo.
Hawa ndio wale wanaojivika sura ya wafu na hujidhihirisha kwetu k**a roho za wale wapendwa wetu waliotuacha, nao hufanya ishara nyingi na maajabu ya uongo.
π _Mungu aliwaonya wana wa Israeli dhidi ya mambo hayo_ *(Kumbukumbu la Torati 18:9-12; Isaya 8:19-20)*.
π Umizimu ni moja ya udanganyifu mkuu ambao shetani anautumia kuwashawishi mamilioni ya watu kuwa upande wake katika siku hizi za mwisho, ndipo watakapoangamia.
*MTEGO WA TELEVISHENI*
π _"Msiwaendee wenye pepo, wala wachawi; msitafute; ili kutiwa unajisi nao; Mimi ndimi BWANA, Mungu wenu_." *(Walawi 19:31).*
π Biblia situkwamba hutuonya dhidi ya kufuata roho mfuba li pia kutoziheshimu.
Kwa namna yoyote ile hatupaswi kujifungamanisha na mambo haya.
π Ndiyo maana namna hizi zote zilipaswa kuwekwa mbali na wana wa Israeli.
Lakini leo shetani amepata njia kwa kila mmoja (hata na wale wanaojidai Wakristo, wakidai kuwa wamejitenga na mambo haya) kuhusika katika umizimu kwa namna moja ama nyingine.
π Zaidi ya njia zote, njia anayoitumia kwa mafanikio zaidi ni televisheni.
βοΈNi matangazo mangapi huonyeshwa kwetu ambayo hutonyesha mambo yanayofanana na hayo ya umizimu?
π Ni mara ngapi tunaona wafu wakiwasiliana na walio hai katika filamu mbalimbali?
π Hivi karibuni nilisimuliwa kuhusu mchezo wa kihindi; kulikuwa na msichana ambaye mama yake alifariki na kisha huyo binti aliona nyota karibu na mwezi, kuashiria kwamba roho ya mama yake ilienda pale na kuwa nyota, cha kushangaza, hata hivyo yule mama alikuwa mdhambi alipokuwa duniani.
Huu ni mfano mdogo tu wa yale tunayoonyeshwa katika skrini hizi.
π Hebu angalia filamu za mashujaa (superheroes films) za Kimarekani, Kihindi, Kichina n.k.
Angalia baadhi ya ishara za kishetani zinazoonyeshwa katika sinema nzima.
π Vipi kuhusu katuni? Ooh! Kuna michezo isiyokuwa na idadi inayofanana na hayo.
π Mungu anaposema tusiwaendee wenye pepo, kwa maana halisiana na roho za mashetani, maana ni dhahiri kuwa ndivyo zilivyo.
π Baadhi ya watu hawa hudai hata kuwasiliana kwa uwazi na mashetani.
Je Mkristo anaweza kuyatupia macho mambo haya?
*Onyo na Hatari*
π Akili yenye kuwaza papo hapo iharaka kudai "*Oh! natambua. Natambua kuwa mambo haya ni ya uongo (ni maigizo tu, si ukweli).* Vile vile siamini mambo hayo."
π K**a hili halina tatizo, basi hakuna maana ya mimi kutumia muda wangu kuandika hili somo
π Kumbuka, Mungu aliwaonya Israeli dhidi ya kujifungamanisha na umizimu.
Ndiyo, hata aliwakataza kuungana na mataifa yafanyayo ibada za sanamu na kuwaruhusu watoto wao waolewe na watoto wa mataifa hayo.
*Sababu ya Kuanguka kwa Waisraeli*
π Nini kiliwapelekea Waisraeli waabudu sanamu?
Ilikuwa ni muungano na mataifa hayo.
π Walijiunga wenyewe na ibada za sanamu, hivyo waliangukia katika kuabudu sanamu.
βοΈJe, walijua mapenzi ya Mungu?
βοΈJe, walijua kwamba Mungu aliwakataza kuabudu sanamu?
Ndiyo, walijua.
π Pengine katika muungano wao na waabudu sanamu walijua kabla, kwamba wasingeanguka, maana walitambua kuwa ibada ya sanamu ilikuwa ni uovu.
Lakini pasipo kutambua, mara nyingi walijikuta wamezama katika ibada ya sanamu.
*Hitimisho na Wito*
π Tabia zetu, imani zetu, kwa kiwango kikubwa zinategemea kile tunachokiweka katika akili zetu. Haijalishi ni mtaalamu kiasi gani, k**a ukielekeza akili yako mahali pa shetani, hakika atakunasa.
π Polepole lakini kwa uhakika zaidi, mfumo huu wa imani unapandikizwa akilini mwetu tukiwatumepumzika bila wasiwasi. Wengi wanapoteza moyo wa dhati wa kumwabudu Mungu kwa sababu ya televisheni.
βοΈNa maana ni hata kutumia mitandao pia, simu. Kwa sasa ni kila mahali. Kuwa makini na kile unachoangalia, kile unachokiweka akilini mwako.
π Sisi tunapaswa kujitenga na uovu, lakini pia kuuchukia.
βοΈJe, kuna yeyote anayedaikuwa anauchukia uasherati ilihali ana utazama kwenye skrini k**a namna fulani ya burudani?
Wewe! unaburudishwa na dhambi! Fikiria malaika watakatifu wakiburudishwa na mambo hayo.
π Je, yeyote anaweza kukataa kwamba leo uasherati au picha za uchi zimechukua nafasi kubwa katika yale yanayoonyeshwa kila siku na televisheni?
βοΈJe, pasipo na shaka yoyote twaweza kusema kuwa mamilioni ya watu wanafanya uzinzi kila siku kwa kuangalia tu?
π Hili ni ombi langu:
_"Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo ya staha, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote yenye kupendeza, yoyote yenye sifa njema; ukiwapo wema wowote, ukiwapo sifa nzuri yoyote, yatafakarini hayo."_ *(Wafilipi 4:8).*
π Endapo akili zetu zitapata mambo mema, nasi pia tutakuwa wasafi.
K**a vile kwa wale ambao moja kwa moja wanahusika katika umizimu wanavyomhitaji Kristo kuokolewa, nasi pia tunamhitaji Kristo.
π Kamba zinazotuunganisha na hizi sinema (matangazo) za televisheni zimekuwa imara kiasi kwamba hatuwezi kuzikata.
πYesu alikuja kwa kusudi hili β kutuweka huru:
π _"Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli_." *(Yohana 8:36)*.
π Maamuzi ndiyo huanza. Amua kujitenga na televisheni pamoja na sinema na michezo yake.
Kisha mfuate Kristo.
Muombe akuweke huru.
Hakika atakuweka huru.
Tayari Yesu alikufa kwa ajili yako.
βοΈKwa nini ufiye dhambini? Jitakase na wasaidie wengine.
π Mungu akubariki.
π Tembelea na ufuatilie ukurasa wetu sasa:
https://www.facebook.com/profile.php?id=61574314941920
π―οΈ *Karibu tujifunze pamoja ili tusije tukadanganywa.*
Ukweli unaokoa, siri hufunuliwa kwa wale wanaotafuta kwa moyo wote.
π *Jiunge nasi WhatsApp kupitia kiungo hiki:*
π² https://whatsapp.com/channel/0029Vb7hYnB7tkjAYUzMFf01
π§ *Wasiliana nasi:* [email protected]
Usikose kuwa sehemu ya jamii inayotafuta ukweli usiobadilika.