π’πˆπ‘πˆ 𝐙𝐀 π”ππ€ππˆπˆ 𝐓𝐕-π’ͺ𝓃𝓁𝒾𝓃𝑒 π»π‘œπ“…π‘’

  • Home
  • Tanzania
  • Arusha
  • π’πˆπ‘πˆ 𝐙𝐀 π”ππ€ππˆπˆ 𝐓𝐕-π’ͺ𝓃𝓁𝒾𝓃𝑒 π»π‘œπ“…π‘’

π’πˆπ‘πˆ 𝐙𝐀 π”ππ€ππˆπˆ 𝐓𝐕-π’ͺ𝓃𝓁𝒾𝓃𝑒 π»π‘œπ“…π‘’ πŸ” SIRI ZA UNABII
Ufahamu wa kina. Ukweli usiofichika. Hapa ndipo mahali sahihi.

Maandalizi ya wakati wa mwisho.

⁉️Je, unatafuta kuelewa kwa undani unabii wa Biblia na maana yake katika maisha ya sasa?

SOMO: TELEVISHENI NA UMIZIMUπŸ’ Moja ya maendeleo makubwa ya teknolojia yaliyoshuhudiwa katika karne iliyopita ni uvumbuzi...
06/04/2026

SOMO: TELEVISHENI NA UMIZIMU

πŸ’ Moja ya maendeleo makubwa ya teknolojia yaliyoshuhudiwa katika karne iliyopita ni uvumbuzi wa televisheni.
Ilipokuwa ikiingia duniani, iliidhinishwa kwa ajili ya mafunisho ya maadili kwamba ingezielimisha jamii.

πŸ’ Hata hivyo, nashangaa mmomonyoko wa maadili leo unachangiwa zaidi na hizi televisheni.
Kwa sasa televisheni zimeanzishwa sana kiasi kwamba katika kila nyumba iliyo na heshima na utaratibu mzuri zinapatikana.

πŸ’ Kwa sasa, zimefanywa kuwa ni hitaji la muhimu kwa kiwango kikubwa.
Ni ngumu katika akili ya yeyote kukataa kwamba maovu mengi yanayosababishwa na hizi skrini tofauti na kuchangia katika maadili mema k**a ilivyodaiwa kwamba ndio makusudi yake.

πŸ’ Miongoni mwa mambo hayo ni picha za nusu uchi, uharifu na udanganyifu mara nyingi huonyeshwa katika sinema mbalimbali na matangazo.
Moja ya mambo ya hatari katika televisheni ni uovu ambao unapandikizwa katika akili na maisha ya mamilioni ya watu, nao ni UMIZIMU.

*Ninimaanaya UMIZIMU?*

πŸ“– Mzizi wa *UMIZIMU* tunaweza kuupata kwa kutazama katika mianzo ya wakati, ambapo malaika aliyeanguka akiwa amejificha katika umbo la nyoka alipotamka maneno yake ya kwanza ya kilaghai kwa mwanadamu;
_"Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa... kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa k**a Mungu, mkijua mema na mabaya_." *(Mwanzo 3:4-5)*.

πŸ“– _Mungu alikuwa ameshawaambia wanadamu kuwa endapo wangekula matunda ya mti uliokatazwa, wangekufa hakika_ *(Mwanzo 2:16,17)*.

πŸ’ Shetani alisema kwamba hawatakufa (akimaanisha kwamba wana roho zisizokufa) bali pia kwamba wangekuwa k**a Mungu.

πŸ’ Umizimu umejengwa katika msingi wa kanuni hizi mbili:
1. *Roho kutokufa na kwamba mtu anapokufa anakua mungu*.
2. *Kupitia msingi huu, shetani amefanya njia ambapo mtu anaweza kuwasiliana na mapepo*.

πŸ“– Biblia iko wazi, kwamba wafu hawajui neno lolote *(Mhubiri 9:5)*.
πŸ’ Shetani hufundisha kwamba mwili hufa bali roho haifi.

✍️ _"Umizimu hufundisha kuwa hapana kifo wala dhambi wala hukumu wala adhabu; kwamba wanadamu ni nusu miungu ambao hawakuanguka dhambini; kwamba tumaini ndilo kanuni kuu; na kwamba mwanadamu huwajibika kwa ajili yake mwenyewe_." *(E.G. White: Patriarchs and Prophets, 688.1)*.

*Historia ya Imani za Umizimu*

πŸ’ Tangu nyakati za zamani, wanadamu walikuwa wakifundishwa kuwa wafu huenda kwenye jua, mwezi au wamekuwa miongoni mwa nyota au sayari.

πŸ’ Katika baadhi ya jamii kuna imani kwamba roho za wafu huingia kwa baadhi ya wanyama; na wengine huamini kuwa wafu hufanya sehemu katika kupatanisha wanadamu kwa Mungu, kwa mfano roho za mababu.

πŸ’ Shetani alitambua kuwa endapo angewafanya wanadamu waamini mambo hayo, hivyo angeweza kuwafanya waabudu sanamu.

πŸ“– Tunasoma kuhusu ibada kwa jua, ibada kwa ng’ombe jike na dume, ibada kwa Mungu kupitia mababu;
Tunasoma kuhusu njia za mawasiliano na mapepo, uchawi β€” wale wanaodai kuwa na mawasiliano na roho za wafu.

πŸ’ Tukiwatunatambua kuwa wafu hawajui lolote, bila shaka ni wazi kuwa watu hawa hawawasiliani na roho zilizokufa bali na malaika walioanguka β€” mapepo.
Hawa ndio wale wanaojivika sura ya wafu na hujidhihirisha kwetu k**a roho za wale wapendwa wetu waliotuacha, nao hufanya ishara nyingi na maajabu ya uongo.

πŸ“– _Mungu aliwaonya wana wa Israeli dhidi ya mambo hayo_ *(Kumbukumbu la Torati 18:9-12; Isaya 8:19-20)*.

πŸ’ Umizimu ni moja ya udanganyifu mkuu ambao shetani anautumia kuwashawishi mamilioni ya watu kuwa upande wake katika siku hizi za mwisho, ndipo watakapoangamia.

*MTEGO WA TELEVISHENI*

πŸ“– _"Msiwaendee wenye pepo, wala wachawi; msitafute; ili kutiwa unajisi nao; Mimi ndimi BWANA, Mungu wenu_." *(Walawi 19:31).*

πŸ’ Biblia situkwamba hutuonya dhidi ya kufuata roho mfuba li pia kutoziheshimu.
Kwa namna yoyote ile hatupaswi kujifungamanisha na mambo haya.

πŸ’ Ndiyo maana namna hizi zote zilipaswa kuwekwa mbali na wana wa Israeli.
Lakini leo shetani amepata njia kwa kila mmoja (hata na wale wanaojidai Wakristo, wakidai kuwa wamejitenga na mambo haya) kuhusika katika umizimu kwa namna moja ama nyingine.

πŸ’ Zaidi ya njia zote, njia anayoitumia kwa mafanikio zaidi ni televisheni.
⁉️Ni matangazo mangapi huonyeshwa kwetu ambayo hutonyesha mambo yanayofanana na hayo ya umizimu?

πŸ’ Ni mara ngapi tunaona wafu wakiwasiliana na walio hai katika filamu mbalimbali?

πŸ’ Hivi karibuni nilisimuliwa kuhusu mchezo wa kihindi; kulikuwa na msichana ambaye mama yake alifariki na kisha huyo binti aliona nyota karibu na mwezi, kuashiria kwamba roho ya mama yake ilienda pale na kuwa nyota, cha kushangaza, hata hivyo yule mama alikuwa mdhambi alipokuwa duniani.
Huu ni mfano mdogo tu wa yale tunayoonyeshwa katika skrini hizi.

πŸ’ Hebu angalia filamu za mashujaa (superheroes films) za Kimarekani, Kihindi, Kichina n.k.
Angalia baadhi ya ishara za kishetani zinazoonyeshwa katika sinema nzima.

πŸ’ Vipi kuhusu katuni? Ooh! Kuna michezo isiyokuwa na idadi inayofanana na hayo.

πŸ“– Mungu anaposema tusiwaendee wenye pepo, kwa maana halisiana na roho za mashetani, maana ni dhahiri kuwa ndivyo zilivyo.

πŸ’ Baadhi ya watu hawa hudai hata kuwasiliana kwa uwazi na mashetani.
Je Mkristo anaweza kuyatupia macho mambo haya?

*Onyo na Hatari*

πŸ’ Akili yenye kuwaza papo hapo iharaka kudai "*Oh! natambua. Natambua kuwa mambo haya ni ya uongo (ni maigizo tu, si ukweli).* Vile vile siamini mambo hayo."

πŸ’ K**a hili halina tatizo, basi hakuna maana ya mimi kutumia muda wangu kuandika hili somo

πŸ“– Kumbuka, Mungu aliwaonya Israeli dhidi ya kujifungamanisha na umizimu.
Ndiyo, hata aliwakataza kuungana na mataifa yafanyayo ibada za sanamu na kuwaruhusu watoto wao waolewe na watoto wa mataifa hayo.

*Sababu ya Kuanguka kwa Waisraeli*

πŸ’ Nini kiliwapelekea Waisraeli waabudu sanamu?
Ilikuwa ni muungano na mataifa hayo.

πŸ’ Walijiunga wenyewe na ibada za sanamu, hivyo waliangukia katika kuabudu sanamu.

⁉️Je, walijua mapenzi ya Mungu?
⁉️Je, walijua kwamba Mungu aliwakataza kuabudu sanamu?

Ndiyo, walijua.

πŸ’ Pengine katika muungano wao na waabudu sanamu walijua kabla, kwamba wasingeanguka, maana walitambua kuwa ibada ya sanamu ilikuwa ni uovu.

Lakini pasipo kutambua, mara nyingi walijikuta wamezama katika ibada ya sanamu.

*Hitimisho na Wito*

πŸ’ Tabia zetu, imani zetu, kwa kiwango kikubwa zinategemea kile tunachokiweka katika akili zetu. Haijalishi ni mtaalamu kiasi gani, k**a ukielekeza akili yako mahali pa shetani, hakika atakunasa.

πŸ’ Polepole lakini kwa uhakika zaidi, mfumo huu wa imani unapandikizwa akilini mwetu tukiwatumepumzika bila wasiwasi. Wengi wanapoteza moyo wa dhati wa kumwabudu Mungu kwa sababu ya televisheni.

⁉️Na maana ni hata kutumia mitandao pia, simu. Kwa sasa ni kila mahali. Kuwa makini na kile unachoangalia, kile unachokiweka akilini mwako.

πŸ’ Sisi tunapaswa kujitenga na uovu, lakini pia kuuchukia.

⁉️Je, kuna yeyote anayedaikuwa anauchukia uasherati ilihali ana utazama kwenye skrini k**a namna fulani ya burudani?

Wewe! unaburudishwa na dhambi! Fikiria malaika watakatifu wakiburudishwa na mambo hayo.

πŸ’ Je, yeyote anaweza kukataa kwamba leo uasherati au picha za uchi zimechukua nafasi kubwa katika yale yanayoonyeshwa kila siku na televisheni?

⁉️Je, pasipo na shaka yoyote twaweza kusema kuwa mamilioni ya watu wanafanya uzinzi kila siku kwa kuangalia tu?

πŸ“– Hili ni ombi langu:
_"Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo ya staha, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote yenye kupendeza, yoyote yenye sifa njema; ukiwapo wema wowote, ukiwapo sifa nzuri yoyote, yatafakarini hayo."_ *(Wafilipi 4:8).*

πŸ’ Endapo akili zetu zitapata mambo mema, nasi pia tutakuwa wasafi.
K**a vile kwa wale ambao moja kwa moja wanahusika katika umizimu wanavyomhitaji Kristo kuokolewa, nasi pia tunamhitaji Kristo.

πŸ’ Kamba zinazotuunganisha na hizi sinema (matangazo) za televisheni zimekuwa imara kiasi kwamba hatuwezi kuzikata.

πŸ’Yesu alikuja kwa kusudi hili β€” kutuweka huru:
πŸ“– _"Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli_." *(Yohana 8:36)*.

πŸ’ Maamuzi ndiyo huanza. Amua kujitenga na televisheni pamoja na sinema na michezo yake.
Kisha mfuate Kristo.
Muombe akuweke huru.
Hakika atakuweka huru.
Tayari Yesu alikufa kwa ajili yako.

⁉️Kwa nini ufiye dhambini? Jitakase na wasaidie wengine.

πŸ™ Mungu akubariki.

πŸ‘‰ Tembelea na ufuatilie ukurasa wetu sasa:
https://www.facebook.com/profile.php?id=61574314941920

πŸ•―οΈ *Karibu tujifunze pamoja ili tusije tukadanganywa.*
Ukweli unaokoa, siri hufunuliwa kwa wale wanaotafuta kwa moyo wote.

πŸ‘‡ *Jiunge nasi WhatsApp kupitia kiungo hiki:*
πŸ“² https://whatsapp.com/channel/0029Vb7hYnB7tkjAYUzMFf01

πŸ“§ *Wasiliana nasi:* [email protected]

Usikose kuwa sehemu ya jamii inayotafuta ukweli usiobadilika.


_πŸ“˜  KUNENA KWA LUGHA β€” KIPAWA CHA MUNGU AU KELELE ZA WANADAMU?_πŸ•―οΈ _Ni sehemu ya mfulurizo wa masomo ya msingi,_πŸ“– _Leo tu...
06/04/2026

_πŸ“˜ KUNENA KWA LUGHA β€” KIPAWA CHA MUNGU AU KELELE ZA WANADAMU?_

πŸ•―οΈ _Ni sehemu ya mfulurizo wa masomo ya msingi,_
πŸ“– _Leo tutachunguza kwa undani maana ya KUNENA KWA LUGHA, mwanzo wake, kusudi lake, na pia tutafunua UPOTOFU uliopenya ndani ya makanisa ya leo._

*🌟 MAANA YA KUNENA KWA LUGHA*

Kunena kwa lugha ni kipawa cha kiroho ambacho mtu hupewa na Roho Mtakatifu ili aweze kusema kwa lugha ambayo hajawahi kujifunza, kwa kusudi la kuujenga mwili wa Kristo au kuwasilisha ujumbe wa Mungu kwa watu wa mataifa tofauti.

πŸ“œ _Matendo 2:4_
_"Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, k**a Roho alivyowajalia kutamka."_

πŸ” Hapa tunaona kuwa lugha walizonena zilikuwa halisi, zenye maana, na watu waliweza kuzisikia na kuelewa (angalia _Matendo 2:6-8_). Hili lilikuwa ni ishara ya kuenea kwa Injili kwa mataifa yote.

*✍️ MWANZO WA KUNENA KWA LUGHA*

Kunena kwa lugha kulianza siku ya Pentekoste, baada ya Yesu kupaa mbinguni. Kipawa hiki kilikuwa sehemu ya uthibitisho wa ujio wa Roho Mtakatifu na mwanzo wa kazi ya kimataifa ya kanisa.

πŸ“œ _Matendo 2:5-8_
_"Basi walikuwako Yerusalemu Wayahudi, watu wacha Mungu, kutoka kila taifa chini ya mbingu... kila mmoja akawasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe."_

βœ… Hii inaonyesha kuwa lugha hizo zilikuwa za mataifa mbalimbali, siyo sauti zisizoeleweka.

*⚠️ UPOTOFU ULIOINGIA KANISANI LEO*

Leo hii, katika baadhi ya makanisa ya kiroho (hasa ya kijumapili), watu hufundishwa au kuhamasishwa kunena kwa lugha zisizoeleweka, mara nyingi kwa kurudia silabi zisizo na maana k**a β€œshandaraba, shandaraba…” wakiamini kuwa huo ni ushahidi wa kuwa na Roho Mtakatifu.

❌ Hii ni kinyume na maandiko, kwani:

- Paulo anasisitiza kuwa kunena kwa lugha bila tafsiri ni bure kwa kanisa.
- Lugha zisizoeleweka hazijengi mtu wala kanisa.
- Kipawa hiki si cha kila mtu, bali hutolewa k**a Roho apendavyo.

*πŸ“– MAELEZO YA MTUME PAULO β€” 1 WAKORINTHO 12, 13, 14*

*πŸ”Ή 1 Wakorintho 12: Kipawa si cha kila mtu*

_"Je, wote hunena kwa lugha? Je, wote hutafsiri?"_ ( _mst. 30_)
➑️ Paulo anaonyesha kuwa si kila mtu atapewa kipawa hiki. Siyo lazima kwa kila muumini.

*πŸ”Ή 1 Wakorintho 13: Upendo ni bora kuliko lugha*

_"Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, k**a sina upendo, nimekuwa shaba iliayo..."_ ( _mst. 1_)
➑️ Kunena kwa lugha bila upendo ni bure. Upendo ni kipawa kikuu kuliko vyote.

*πŸ”Ή 1 Wakorintho 14: Nidhamu na tafsiri ni muhimu*

- _"Yeye anenaye kwa lugha hajisemei na watu, bali husema na Mungu; maana hakuna mtu amwelewapo."_ ( _mst. 2_)
- _"Lakini katika kanisa napenda kusema maneno matano kwa akili yangu... kuliko kusema maneno elfu kwa lugha."_ ( _mst. 19_)
- _"Ikiwa hakuna mkalimani, na anyamaze kanisani."_ ( _mst. 28_)

βœ… Paulo anasisitiza kuwa kunena kwa lugha kunapaswa kuwa na tafsiri, na k**a hakuna tafsiri, ni bora kunyamaza.

*KUNENA KWA LUGHA β€” KIPAWA CHA MAANA, SI KELELE*

Kunena kwa lugha ni zawadi ya kipekee kutoka kwa Mungu, lakini si kila sauti isiyoeleweka ni lugha ya kiroho. Kipawa hiki kilikuwa na kusudi maalum β€” kueneza Injili kwa mataifa na kujenga kanisa. Leo hii, tunapaswa kuwa waangalifu tusije tukapotoshwa na hisia au desturi zisizo na msingi wa maandiko.

πŸ“– _"Roho huwapeni kila mmoja peke yake k**a apendavyo."_ β€” _1 Wakorintho 12:11_


πŸ“– _"Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani, k**a vile ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu."_
*1 Wakorintho 14:33 (SUV):*
---

πŸ“² _Endelea kufuatilia mfululizo huu wa kina kupitia channel yetu ya WhatsApp:_
πŸ‘‰ [SIRI ZA UNABII](https://whatsapp.com/channel/0029Vb7hYnB7tkjAYUzMFf01)

πŸ“’  SIRI ZA UNABII MEDIAWapendwa wafuatiliaji na wanafunzi wa kweli,Katika nyakati hizi za mwisho ambapo maarifa ya kweli...
05/04/2026

πŸ“’ SIRI ZA UNABII MEDIA

Wapendwa wafuatiliaji na wanafunzi wa kweli,
Katika nyakati hizi za mwisho ambapo maarifa ya kweli yanahitajika zaidi kuliko wakati mwingine wowote, tunawakaribisha kwa moyo mkunjufu kujiunga nasi katika ukurasa wetu rasmi wa Facebook.

Kupitia jukwaa hili, utapata mafundisho ya kina ya Neno la Mungu, uchambuzi wa unabii, na kweli zitakazokuimarisha kiroho na kukuandaa kwa wakati ujao.

πŸ‘‰ Tembelea na ufuatilie ukurasa wetu sasa:
https://www.facebook.com/profile.php?id=61574314941920

Usikose kuwa sehemu ya jamii inayotafuta ukweli usiobadilika.

πŸ‘‰ Tembelea na ufuatilie ukurasa wetu sasa:
https://www.facebook.com/profile.php?id=61574314941920

πŸ•―οΈ *Karibu tujifunze pamoja ili tusije tukadanganywa.*
Ukweli unaokoa, siri hufunuliwa kwa wale wanaotafuta kwa moyo wote.

πŸ‘‡ *Jiunge nasi WhatsApp kupitia kiungo hiki:*
πŸ“² https://whatsapp.com/channel/0029Vb7hYnB7tkjAYUzMFf01

πŸ“§ *Wasiliana nasi:* [email protected]

Usikose kuwa sehemu ya jamii inayotafuta ukweli usiobadilika.




#*sirizaunabii*
#*ukweliunaokuwekahuru*

πŸ“’ SECRETS OF PROPHECY MEDIABeloved followers and sincere students,In these last days, when true knowledge is needed more...
05/04/2026

πŸ“’ SECRETS OF PROPHECY MEDIA

Beloved followers and sincere students,
In these last days, when true knowledge is needed more than ever before, we warmly invite you to join us on our official page.

Through this platform, you will receive in-depth teachings of the Word of God, prophetic insights, and truths that will strengthen you spiritually and prepare you for the future.

πŸ‘‰ Visit and follow our page now:
https://www.facebook.com/profile.php?id=61574314941920
https://www.facebook.com/profile.php?id=61574314941920

Don’t miss the opportunity to be part of a community that seeks unchanging truth.


```KUFUNGWA KWA KIPINDI CHA REHEMA ZA MUNGU```*Kipindi cha Rehema*πŸ’ Hiki ni kipindi walichopewa wanadamu kuacha dhambi n...
05/04/2026

```KUFUNGWA KWA KIPINDI CHA REHEMA ZA MUNGU```

*Kipindi cha Rehema*

πŸ’ Hiki ni kipindi walichopewa wanadamu kuacha dhambi na kumrudia Mungu, wajipatanishe naye na kushika maagizo yake ili waokolewe.
Mungu atakapofunga kipindi hiki cha rehema haitawezekana tena kwa mwanadamu awaye yote kusamehewa dhambi zake. Hatima ya umilele wa kila mmoja itakuwa imekwishaamriwa.

*Mungu ni Mwingi wa Rehema*

πŸ’ Mungu ni mwingi wa rehema, husamehe wadhambi, wanaovunja maagizo na amri zake wanaotubu na kuacha uovu wao wote.

πŸ’Ingawa yeye anayajua maovu yetu, yeye hatoi adhabu stahili wakati wote.

πŸ“– *Kutoka 34:5-7* β†’ _β€œβ€¦ Mungu mwingi wa huruma … si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema … mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe …”_

πŸ’ Aya hizi zinasema kuwa pamoja na wingi wa huruma na rehema zake, Mungu hawezi kuacha kumhesabia hatia mtu awaye yote ambaye hataki kutubu na kuuacha uovu wake.
Kwa hiyo rehema za Mungu zinatutaka wote kuacha dhambi na kujipatanisha na maandiko yake.

πŸ“– *Mika 6:8* β†’ _β€œEe mwanadamu, yeye amekuonesha yaliyo mema; na Bwana anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!”_

πŸ“– *Mika 7:18* β†’ _β€œNi nani aliye Mungu k**a wewe, mwenye kusamehe uovu, na kuliachilia kosa la watu wa urithi wake waliosalia? Hashiki hasira yake milele, kwa maana yeye hufurahia rehema. Atarejea na kutuhurumia; atayakanyaga maovu yetu; nawe utazitupa dhambi zao zote katika vilindi vya bahari.”_

*Upatanisho na Mungu*

πŸ’ Rehema za Mungu, dhambi za wote wanaotubu husafishwa kwa damu ya Kristo (Yohana 1:29).

πŸ’Kwa miaka takribani 2000 sasa, Yesu amekuwa akifanya kazi k**a kuhani mkuu mbinguni akiwaombea msamaha wadhambi wanaotubu na kuacha dhambi, na kuwapatanisha na Mungu Baba.

πŸ“– *1 Yohana 2:1-2* β†’ _β€œβ€¦ tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.”_

πŸ“– *Warumi 2:4; 2 Petro 3:9* β†’ _β€œAu waudharau wingi wa wema wake na ustahimilivu wake na uvumilivu wake, usijue ya kuwa wema wa Mungu wakuvuta upate kutubu?”_

```Vipindi na Matukio Ambayo Rehema Zinafungwa```

1. Mtu Anapokufa

πŸ’ Mtu anapokufa mlango wake wa rehema unakuwa umefungwa, anasubiri utekelezaji wa hukumu ya mwisho.

πŸ“– *Waebrania 9:29* β†’ _β€œNa k**a vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu.”_

πŸ’ Fundisho la kwamba wafu husafishwa dhambi zao ndogo ndogo _*β€œtoharani”*_ kabla ya kuchukuliwa mbinguni ni la kibinadamu na halina msingi katika Maandiko.
Asili yake ni ya umizimu na ya wabudha wa kichina.

2. Kukufuru Roho Mtakatifu

πŸ’ Mtu anapomkufuru Roho Mtakatifu mlango wa rehema kwake unafungwa.
Anakuwa ametenda dhambi isiyosameheka, yaani dhambi ya mauti (1 Yohana 5:16-17).

πŸ“– *Mathayo 12:31-32* β†’ _β€œKwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa … hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao.”_

πŸ“– *Mwanzo 6:3* β†’ _β€œβ€¦ Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele …”_

✍️ Ellen G. White: _*β€œKila siku tumekuwa tukishirikiana na watu wanaokwenda hukumuni. Kila siku huenda imekuwa ndiyo mstari unaotenganisha roho fulani; mtu fulani huenda ndiyo amefanya maamuzi yatakayoamua hatima yake ya umilele …”*_

3. Atakapomaliza Kazi ya Kuwapatanisha Wanadamu na Mungu

πŸ’ Yesu, kuhani wetu mkuu, atakapomaliza kazi yake kuwaombea na kuwapatanisha wanadamu na Mungu, mlango wa rehema utafungwa kwa watu wote.

πŸ“– *Ufunuo 22:11* β†’ _β€œMwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.”_

πŸ’ Atakaposema _*β€œImekwisha”*_ hatima ya umilele wa kila mtu itakuwa imeamriwa.
Ghadhabu kali ya Mungu, mapigo makali yataanza kuwaangukia waliokataa maonyo na kuyafuata mafundisho ya uongo.
Itakuwa kilio kikuu na kusaga meno. Haitawezekana tena kabisa kuokolewa.

*Hitimisho*

πŸ’ Unabii wa siku za mwisho unaonesha kuwa fursa hii ya rehema iko karibu kufungwa.
Hivi karibuni Yesu atamaliza kazi yake ya kuwaombea na kuwapatanisha wanadamu na Mungu.

πŸ“– *Ufunuo 18:1-5* β†’ _β€œTokeni kwake (Babeli), enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.”_

πŸ’ Mwenyezi Mungu anatusihi sisi sote, anakusihi wewe msomaji wa kitabu hiki, anawasihi watu wote watoke katika mafundisho ya kutunga, yanayokinzana na Biblia takatifu.
Anatutaka tutoke katika ibada na maombi ya wafu, ibada za sanamu, sabato bandia, ubatizo bandia, vyakula najisi na kila aina ya imani inayokinzana na Maandiko.

πŸ“– *Ufunuo 18:5* β†’ _β€œKwa maana dhambi zake zimefika hata mbinguni, na Mungu amekumbuka maovu yake.”_

πŸ“– *Matendo 22:16* β†’ _β€œBasi sasa, unakawilia nini? Simama, ubatizwe, ukaoshe dhambi zako, ukiliitia jina lake.”_

πŸ“– *Marko 16:16* β†’ _β€œAaminiye na kubatizwa ataokoka, asiyeamini atahukumiwa.”_

✝️ Amini kweli ya Mungu uokolewe!

πŸ‘‰ Tembelea na ufuatilie ukurasa wetu sasa:
https://www.facebook.com/profile.php?id=61574314941920

πŸ•―οΈ *Karibu tujifunze pamoja ili tusije tukadanganywa.*
Ukweli unaokoa, siri hufunuliwa kwa wale wanaotafuta kwa moyo wote.

πŸ‘‡ *Jiunge nasi WhatsApp kupitia kiungo hiki:*
πŸ“² https://whatsapp.com/channel/0029Vb7hYnB7tkjAYUzMFf01

πŸ“§ *Wasiliana nasi:* [email protected]

Usikose kuwa sehemu ya jamii inayotafuta ukweli usiobadilika.


MWISHO...```Watu wa Mungu Hawatapotoshwa``` πŸ™ Lakini watu wa Mungu hawatapotoshwa. Mafundisho ya kristo huyu wa uongo ha...
05/04/2026

MWISHO...

```Watu wa Mungu Hawatapotoshwa```

πŸ™ Lakini watu wa Mungu hawatapotoshwa. Mafundisho ya kristo huyu wa uongo hayapatani na Maandiko Matakatifu. Baraka zake zinatolewa kwa wale wanaomwabudu mnyama na sanamu yake, kundi lile lile ambalo Biblia inasema watakinywea kikombe cha ghadhabu ya Mungu isiyochanganywa na maji.

⚠️ Zaidi ya hayo, Shetani hataruhusiwa kufanya udanganyifu wa namna ujio wa Kristo utakavyokuwa. Kristo amewaonya watu wake dhidi ya udanganyifu juu ya jambo hili: _β€œKwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, k**a yamkini, hata walio wateule... Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki. Kwa maana k**a vile umeme utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.”_
πŸ“– *Mathayo 24:24-27; Mathayo 25:31; Ufunuo 1:7; 1 Wathesalonike 4:16-17*

πŸ“– Ujio huu, hakuna uwezekano wa kuupotosha. Utashuhudiwa na dunia yote.

πŸ“š Ni wanafunzi tu wenye bidii ya kujifunza Maandiko ambao wamepokea upendo wa kweli watakaosimama imara dhidi ya udanganyifu unaouteka ulimwengu. Kwa ushuhuda wa Biblia hawa watamtambua mdanganyifu katika hila zake.

*Wakati wa Kukimbia*

🏞️ Kwa vile tamko litakalotolewa na viongozi mbalimbali wa ulimwengu wa Ukristo dhidi ya washika amri litapelekea kuondolewa kwa ulinzi wa serikali na kuwaacha mikononi mwa wale wanaotaka kuwaharibu; watu wa Mungu watakimbia kutoka kwenye miji na vijiji kujiunga pamoja kwenye makundi, wakiishi mahali palipo ukiwa na upweke kabisa.

⛰️ Wengi watatafuta makao katika maeneo ya milimani, k**a Wakristo wa mabonde ya Piedmont. Lakini watu wengi kutoka mataifa yote na madaraja mbalimbali, wa hali ya juu na ya chini, maskini na matajiri, weupe na weusi, watatupwa katika utumwa usio wa haki na wa kikatili.

⛓️ Wapendwa wa Bwana watapitia katika siku za kuchosha wakifungwa magerezani, watahukumiwa kuchinjwa, wataachwa wafe gizani katika magereza ya ardhini.

*Je, Bwana Atawasahau?*

❓ Je, Bwana atawasahau watu wake katika saa hii ya kujaribiwa? Je, aliwasahau watu wake waaminifu Nuhu, Lutu, Yusufu, Eliya, Yeremia au Danieli?

πŸ‘Ό Japo adui awatupa gerezani, lakini kuta za gereza la ardhini, hataweza kukata mawasiliano kati ya roho zao na Kristo. Malaika watawaijia kwenye vyumba hivyo vyenye upweke.

🌟 Gereza litakuwa k**a ikulu, kuta zitaangaziwa nuru k**a ilivyokuwa kwa Paulo na Sila walipoimba usiku wa manane katika gereza kule Filipi.

*Hukumu ya Mungu*

βš–οΈ Hukumu ya Mungu itawaangukia wale wanaotafuta kuwaangamiza watu wake. Kwa Mungu hukumu ni _β€œtendo la ajabu.”_
πŸ“– *Isaya 28:21; Ezekieli 33:11; Kutoka 34:6-7; Nahumu 1:3*

πŸ”₯ Taifa ambalo amelivumilia na ambalo limekijaza kikombe cha uharibifu wake hatimaye litakunywa kikombe cha ghadhabu ya Mungu kisichochanganywa na rehema.

*Mapigo ya Mwisho*

πŸŒ‘ Kristo atakapoacha kufanya upatanisho katika patakatifu pa mbinguni, ghadhabu isiyochanganywa na maji dhidi ya wale wanaomwabudu mnyama itamwagwa.
πŸ“– *Ufunuo 16:2-6*

🩸 Mapigo kule Misri yalifanana na hukumu zile zilizokuwa za kutisha ambazo ndizo zitakazoupata ulimwengu kabla ya ukombozi wa mwisho wa watu wa Mungu.

β˜€οΈ Katika pigo lililofuata, jua linapewa uwezo _β€œili kuwaunguza wanadamu kwa moto.”_
πŸ“– *Ufunuo 16:8-9; Yoeli 1:11-12, 18-20*

*Watu wa Mungu Watalindwa*

πŸ•ŠοΈ Watu wa Mungu hawataachwa waangamie japokuwa wanateseka na kutaabika kwa sababu ya mambo mema. Malaika watawahudumia kwa mahitaji yao.
πŸ“– *Isaya 33:16; Isaya 41:17*

πŸ˜” Lakini katika macho ya kibinadamu itaonekana kuwa watu wa Mungu watakuwa radhi kutia muhuri ushuhuda wa maisha yao kwa damu yao, k**a walivyofanya wafia dini waliowatangulia.

*Makundi ya Malaika Wanalinda*

πŸ‘Ό Malaika wamewekwa katika vituo kuwalinda wale ambao wamelitunza neno la subira la Kristo. Watakuwa wameshuhudia matatizo na kuwasikia wakitoa maombi yao.

βš”οΈ Watasubiri kauli ya K**anda wao ya kuwadaka kutoka kwenye hatari yao. Lakini itawabidi wasubiri kwa kitambo kidogo.
πŸ“– *Mathayo 20:20-23*

πŸ›‘οΈ Japokuwa tamko kuu litakuwa limekwisha weka muda maalum ambapo washika sheria watauawa, adui zao katika baadhi ya matukio watawashambulia kuondoa uhai wao. Lakini hakuna atakayeweza kuwapita walinzi watakaokuwa wameizingira kila nafsi yenye uaminifu.

*Ushuhuda wa Malaika*

πŸ“œ Katika vipindi vyote vya historia malaika wametekeleza majukumu muhimu katika mambo ya wanadamu. Wameukubali ukarimu waliotendwa katika nyumba za watu, wamekuwa viongozi kwa wasafiri wa usiku, wamefungua milango ya magereza na kuwaweka huru watumishi wa Bwana.

πŸͺ¨ Waliliondoa jiwe kwenye kaburi la Mwokozi. Malaika huenda kwenye makusanyiko ya watu waovu, k**a walivyoenda Sodoma kujua ikiwa wamevuka ukomo wa uvumilivu wa Mungu.

🌍 Kwa ajili ya watumishi wachache wanaomtumikia Mungu kwa uhalisi, anazuia majanga na kudumisha amani kwa watu wengi.

*Tumaini la Mwisho*

πŸŒ… Kwa hamu kubwa, watu wa Mungu wanasubiria dalili ya mfalme wao ajaye. Kadiri watu wanaoishindana na Mungu wanavyoendelea kusihi mbele zake, mbingu zitang’aa kwa mapambazuko ya milele.

🎢 K**a ilivyo sauti tamu ya nyimbo za malaika, ndivyo yatakavyokuwa maneno yatakayoingia katika sikio: _β€œMsaada unakuja.”_

πŸ—£οΈ Sauti ya Kristo itatoka kwenye malango yaliyo wazi: _β€œTazama, niko pamoja nanyi. Msiogope. Nimepigana vita kwa niaba yenu, na kwa jina langu ninyi ni zaidi ya washindi.”_

*Ukombozi*

✝️ Mwokozi mpendwa atatuma msaada wakati tutakapouhitaji. Wakati wa taabu utakuwa ni wakati wa mateso ya kutisha kwa watu wa Mungu, lakini kila muumini wa kweli ataona kwa imani upinde wa ahadi za Mungu ukimzunguka.
πŸ“– Isaya 51:11

πŸ›‘οΈ Kristo amesema: _β€œNjoni, watu wangu, ingia wewe ndani ya vyumba vyako, ukafunge mlango nyuma yako ujifiche kitambo kidogo, mpaka ghadhabu hii itakapopita. Kwa maana, tazama, Bwana anakuja kutoka mahali pake, ili kuwaadhibu wakaao duniani, kwa sababu ya uovu wao.”_
πŸ“– Isaya 26:20-21

🌟 Kwa wale ambao watakuwa wamesubiri kwa uvumilivu ujio wa Bwana na wale ambao majina yao yameandikwa kwenye kitabu cha uzima, ukombozi wao utakuwa wenye utukufu.

πŸ“Œ MwishoπŸ‘‰ Tembelea na ufuatilie ukurasa wetu sasa:
https://www.facebook.com/profile.php?id=61574314941920

πŸ•―οΈ *Karibu tujifunze pamoja ili tusije tukadanganywa.*
Ukweli unaokoa, siri hufunuliwa kwa wale wanaotafuta kwa moyo wote.

πŸ‘‡ *Jiunge nasi WhatsApp kupitia kiungo hiki:*
πŸ“² https://whatsapp.com/channel/0029Vb7hYnB7tkjAYUzMFf01

πŸ“§ *Wasiliana nasi:* [email protected]

Usikose kuwa sehemu ya jamii inayotafuta ukweli usiobadilika.


_SEHEM YA PILI...._ *Mungu Analaumiwa Kwa Sababu ya Maumivu*πŸ˜” Lakini uchungu ambao watu wa Mungu wataupata hautakuwa hof...
05/04/2026

_SEHEM YA PILI...._

*Mungu Analaumiwa Kwa Sababu ya Maumivu*

πŸ˜” Lakini uchungu ambao watu wa Mungu wataupata hautakuwa hofu ya mateso. Watahofu kuwa kwa sababu ya makosa yao fulani, ahadi ya Mwokozi: _β€œMimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi.”_ haitatimia kwao. Wakidhihirisha kutostahili kwao kwa sababu ya upungufu katika tabia zao, jina takatifu la Mungu litatukanwa.
πŸ“– *Ufunuo 3:10*

πŸ™ Wataikumbuka toba ya zamani juu ya dhambi zao nyingi na wataomba ahadi ya Mwokozi: _β€œAu azishike nguvu zangu, Afanye amani nami; Naam, afanye amani nami.”_ Hata k**a watasumbuliwa na mateso, msongo na huzuni; hawataacha kuomba.
πŸ“– *Isaya 27:5*

🀲 Watamshika Mungu k**a Yakobo alivyomshika malaika, na lugha ya roho zao itakuwa: _β€œSitakuachia uende, mpaka unibariki.”_

*Kufutwa kwa Dhambi*

βš–οΈ Katika kipindi cha taabu, k**a watu wa Mungu watakuwa na dhambi ambazo hawakutubu, ambazo zitatokea mbele yao wakati wakiwa katika ile hofu na uchungu; kwa hakika watashindwa. Kukata tamaa kutaondoa imani yao, na hawataweza kumsihi Mungu awaokoe.

✨ Lakini hawatakuwa na makosa yoyote yatakayohitaji kufunuliwa. Dhambi zao zitakuwa zimetangulia kwenye hukumu na kuondolewa, na hawataweza kuzikumbuka.

πŸ”₯ Katika kushughulika na Yakobo, Bwana ameonesha kwamba hawezi kuvumilia uovu. Wale wote wanaotoa udhuru au kuzificha dhambi zao na kuruhusu ziendelee kuwepo kwenye vitabu vya mbinguni bila kutubu na kusamehewa wanashindwa na Shetani.

⏳ Wanaochelewa kufanya maandalizi hivi sasa hawatapata nafasi hiyo wakati wa taabu. Hali ya watu wote k**a hao haina matumaini.

*Historia ya Yakobo*

πŸ“– Historia ya Yakobo ni uhakika pia kwamba Mungu hatawatupa wale ambao baada ya kudanganyika dhambini, wameamua kurudi kwake kwa toba ya kweli.

πŸ‘Ό Mungu atatuma malaika kuwafariji wakati wa shida. Jicho la Bwana lipo juu ya watu wake. Miali ya moto wa tanuru inaonekana karibu itawaangamiza, lakini msafishaji atawatoa wakiwa k**a dhahabu iliyojaribiwa motoni.

*Imani Inayostahimili*

πŸ’ͺ Wakati wa mateso na maumivu makali ulio mbele yetu utahitaji imani inayoweza kustahimili uchovu, kuchelewa, na njaa, imani ambayo haitazimia hata k**a itajaribiwa vikali.

πŸ™ Ushindi wa Yakobo ni ushahidi wa nguvu ya maombi yasiyokoma. Wale wote watakaozishikilia ahadi za Mungu k**a alivyofanya Yakobo, watashinda k**a alivyoshinda.

βš”οΈ Kupigana mieleka na Mungu β€” ni wachache kiasi gani wale wanaojua maana yake! Wakati mawimbi ya mashaka yanapomwathiri muombaji, ni wachache sana wanaoshikilia kwa imani ahadi za Mungu.

😟 Wale ambao wanaonesha imani kidogo sasa, wako katika hatari kuu ya kuangukia kwenye uwezo wa Shetani wa udanganyifu. Na hata k**a watastahimili jaribio watatumbukizwa katika mateso mazito wakati wa taabu, hii ni kwa sababu hawakuifanya kuwa tabia yao kumtumainia Mungu.

*Wito wa Kujiandaa*

πŸ“– Mara nyingi taabu inakuwa kubwa wakati inapotarajiwa kuliko katika uhalisia, lakini hili sio kweli kuhusiana na Zahama iliyo mbele yetu.

πŸ•ŠοΈ Wakati huu ambapo Kuhani Mkuu anafanya upatanisho kwa ajili yetu, yatupasa tujitahidi kuwa wakamilifu katika Kristo. Mwokozi wetu hakufikishwa hatua ya kuanguka katika jaribu hata kwa wazo moja.
πŸ“– *Yohana 14:30*

✝️ Ni katika maisha haya ndipo tunatakiwa kujitenga na dhambi, kwa njia ya imani katika damu ya upatanisho ya Kristo. Mwokozi wetu wa thamani anatualika tujiunge naye, tuunganishe udhaifu wetu na nguvu zake, tuunganishe kutostahili kwetu na kufaa kwake.

*Udanganyifu wa Mwisho*

πŸ‘Ώ Kazi ya Shetani ya udanganyifu na uharibifu itafikia katika kilele chake wakati wa taabu. Mionekano ya kutisha ya kiumbe asiye wa kawaida itafunuliwa angani, katika sura ya uwezo wa maShetani wa kutenda miujiza.

🌍 Roho za maShetani zitaenda kwa _β€œwafalme wa dunia”_ na duniani kote kuwashawishi ili waungane na Shetani katika jitihada zake za mwisho dhidi ya serikali ya mbinguni.

πŸ•ŠοΈ Watu watainuka wakijifanya kuwa wao ni Kristo mwenyewe. Watafanya miujiza ya uponyaji na kukiri kwamba wana ufunuo kutoka mbinguni unaopingana na Maandiko.

⚠️ K**a tendo la mwisho katika igizo kuu la udanganyifu, Shetani mwenyewe atamwigiza Kristo. Kanisa kwa muda mrefu limetazamia kuja kwa Mwokozi k**a utimilifu wa matumaini yote.
πŸ“– *Ufunuo 1:13-15*

🌟 Utukufu utakaomzunguka Shetani haupitwi na kitu chochote ambacho macho ya mwanadamu yamewahi kukiona. Sauti kuu ya ushindi itasikika: _β€œKristo amekuja!”_ Watu wataanguka kifudifudi mbele zake.

πŸ—£οΈ Naye atainua mikono yake na kuwabariki. Sauti yake ni laini lakini tamu. Kwa kutumia sauti ya huruma ataeleza baadhi ya kweli zile zile za mbinguni ambazo Mwokozi alizitamka.

πŸ’” Ataponya magonjwa, kisha kwa kujifanya ana tabia ya Kristo, atadai kwamba aliibadilisha Sabato kuwa Jumapili. Atasema kwamba wale wanaoishika siku ya saba takatifu wanalikufuru jina lake.

πŸ‘Ώ Huu ni udanganyifu mkubwa unaoangusha. Wengi watausikiliza uchawi huu, wakisema: _β€œHuu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu.”_
πŸ“– *Matendo 8:10*

πŸ“Œ Inaendelea...

πŸ‘‰ Tembelea na ufuatilie ukurasa wetu sasa:
https://www.facebook.com/profile.php?id=61574314941920

πŸ•―οΈ *Karibu tujifunze pamoja ili tusije tukadanganywa.*
Ukweli unaokoa, siri hufunuliwa kwa wale wanaotafuta kwa moyo wote.

πŸ‘‡ *Jiunge nasi WhatsApp kupitia kiungo hiki:*
πŸ“² https://whatsapp.com/channel/0029Vb7hYnB7tkjAYUzMFf01

πŸ“§ *Wasiliana nasi:* [email protected]

Usikose kuwa sehemu ya jamii inayotafuta ukweli usiobadilika.


Address

Arusha
001

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when π’πˆπ‘πˆ 𝐙𝐀 π”ππ€ππˆπˆ 𝐓𝐕-π’ͺ𝓃𝓁𝒾𝓃𝑒 π»π‘œπ“…π‘’ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category