13/01/2022
Leo hii ntakwambia mambo kuhusu umuhimu wa kuwa na tovuti katika
biashara yako au huduma yoyote ile:
1. 93% YA MAAMUZI YA MTEJA KUHUSU MANUNUZI HUANZIA MITANDAONI:
Ili kuweza kupata wateja wapya, huna budi kuelewa watu
huenda wapi kutafuta vitu k**a suppliers, bidhaa na huduma
mbalimbali kabla ya kufanya manunuzi.
2. UWELEDI (PROFESSIONALISM)
K**a una malengo ya kuifanya biashara yako iwe kubwa duniani, halafu
bado huna tovuti rasmi, jua kuna sehemu kubwa ya soko haitakupa
kipaumbele watakapokuwa na uhitaji wa huduma/bidhaa ulizonazo.
3. KUPATIKANA KWA URAHISI
Hebu fikira ila ahueni ya kupata kila unachokihitaji kwa urahisi,
tena kupitia katika simu yako tu iliyo kiganjani kwako.
4. TANGAZO LA BURE MUDA WOTE
Tovuti yako inapokuwa hewani, maana yake biashara yako ipo wazi
na inajitangaza muda wote na kufika sehemu zote duniani ambapo
huduma ya internet inapatikana.
5. KUTENGENEZA MABALOZI (TESTIMONIALS)
Nafahamu wafanyabiashara wengi ambao hulazimika kuonyesha
shuhuda/testimonials katika kurasa zao mara kwa mara ili
kuendelea kupata wateja wapya zaidi, ni jambo jema kabisa.
6. UAMINIFU (TRUST)
Hamna kitu muhimu katika uendeshaji wa biashara na kukuza
mahusiano na mteja k**a UAMINIFU.
7. THAMANI INAYODUMU
Uzuri/Faida moja muhimu kuhusu tovuti ni kwamba, unapoitengeneza
una uhakika wa kuimiliki milele na kuifanyia marekebisho muda wowote
itakapohitajika kufanya hivyo.
8. HUDUMA BINAFSI YA MSAADA KWA WATEJA
Tovuti yako inapokuwa hewani 24/7 una uhakika na kutoa huduma bora
kwa mteja mmoja mmoja kuhusu maulizo ya huduma/bidhaa ulizonazo, bei,
ushauri nakadhalika.
ZINGATIA HILI:
Katika ulimwengu wa kisasa wa Dijitali, ili kutengeneza nafasi ya
kupata wateja zaidi huna budi kuwa na Tovuti hai itakayobeba taarifa
muhimu k**a jina la biashara, anuani, mawasiliano na maudhui kuhusu
huduma na bidhaa zako. Zaidi, weka pia matumizi ya SEO kuongeza kasi.