09/06/2026
Jana, kampuni yetu ilikuwa miongoni mwa washiriki katika kikao kilichoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani, kikijumuisha wadau mbalimbali wa sekta ya ardhi.
Katika kikao hicho, Mkuu wa Wilaya alitoa maelekezo, mbinu na ushauri muhimu unaolenga kuimarisha na kukuza sekta ya ardhi kwa manufaa ya wadau wote na maendeleo ya jamii kwa ujumla.
Sisi k**a DCG, tumeyapokea maelekezo hayo kwa uzito mkubwa na tumejipanga kuyafanyia kazi kwa vitendo ili kuendelea kutoa huduma bora na kuchangia maendeleo endelevu ya sekta ya ardhi nchini.