13/07/2026
NHC YASHIRIKI MAONESHO YA KIMATAIFA YA SARATANI YA MFUMO WA FAHAMU DAR ES SALAAM
Dar es Salaam, Julai 2026 β Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) linashiriki maonesho ya siku tatu yanayoambatana na Mkutano wa Kimataifa wa Wataalam wa Magonjwa ya Saratani ya Mfumo wa Fahamu wa Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara (SNOSSA 2026), unaofanyika katika Hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam. Mkutano huo unawakutanisha wataalam wa afya, watafiti, wadau wa maendeleo na washiriki kutoka mataifa mbalimbali kujadili namna ya kuimarisha huduma za neuro-oncology barani Afrika.
Maonesho hayo yalifunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ambaye alisisitiza dhamira ya Serikali ya kuendelea kuimarisha huduma za afya kupitia uwekezaji katika uchunguzi, matibabu ya saratani, utafiti na vifaa tiba kuanzia ngazi ya msingi hadi hospitali za rufaa za taifa.
Kupitia ushiriki wake, NHC linaonesha uwezo wake katika kubuni na kutekeleza miradi ya kisasa ya miundombinu ya afya ikiwemo hospitali, vituo vya afya, maabara, majengo ya tiba na miundombinu mingine ya huduma za jamii inayokidhi viwango vya kitaifa na kimataifa.
Ushiriki wa NHC katika maonesho haya unaakisi dhamira ya Shirika ya kuendelea kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali katika kujenga miundombinu imara inayochangia utoaji wa huduma bora za afya na maendeleo endelevu ya Taifa.
**NHC β Tunajenga Taifa Letu.**