National Housing Corporation

National Housing Corporation Government organisation, Real Estate Developer NHC is under the Ministry of Lands, Housing and Settlements Development.

The current National Housing Corporation is the outcome of the decision of the Government to dissolve the Register of building (RoB) through Act of Parliament No.2 of 1990, which vested its responsibilities with the NHC. The former NHC was established by Act of Parliament No.45 of 1962, while RoB was established by Act No.13 of 1971. The Ministry is represented by the Board of Directors which is r

esponsible for the corporate policies and strategies. The day to day management of NHC's business is overseen by the Director General who is responsible to the Board of Directors. Effective from July, 1994, the Corporation's portfolios have been divided into profit centers which are income generating and self-sustaining directorates and cost centers which play a supportive role. This role mandates the NHC to undertake an array of business.
- Construction of houses for sale.
- Construction of buildings as part of approved scheme.
- Provision of facilitating the provision of building materials, components, concrete article and other related articles.
- Business of building contractors, planners or consultants.
- Renting out and managing houses or properties built by the corporation and those acquired by the government.
- Carrying out other activities related to construction of houses or other building built or acquired by the corporation.

NHC YASHIRIKI MAONESHO YA KIMATAIFA YA SARATANI YA MFUMO WA FAHAMU DAR ES SALAAMDar es Salaam, Julai 2026 – Shirika la N...
13/07/2026

NHC YASHIRIKI MAONESHO YA KIMATAIFA YA SARATANI YA MFUMO WA FAHAMU DAR ES SALAAM
Dar es Salaam, Julai 2026 – Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) linashiriki maonesho ya siku tatu yanayoambatana na Mkutano wa Kimataifa wa Wataalam wa Magonjwa ya Saratani ya Mfumo wa Fahamu wa Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara (SNOSSA 2026), unaofanyika katika Hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam. Mkutano huo unawakutanisha wataalam wa afya, watafiti, wadau wa maendeleo na washiriki kutoka mataifa mbalimbali kujadili namna ya kuimarisha huduma za neuro-oncology barani Afrika.
Maonesho hayo yalifunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ambaye alisisitiza dhamira ya Serikali ya kuendelea kuimarisha huduma za afya kupitia uwekezaji katika uchunguzi, matibabu ya saratani, utafiti na vifaa tiba kuanzia ngazi ya msingi hadi hospitali za rufaa za taifa.
Kupitia ushiriki wake, NHC linaonesha uwezo wake katika kubuni na kutekeleza miradi ya kisasa ya miundombinu ya afya ikiwemo hospitali, vituo vya afya, maabara, majengo ya tiba na miundombinu mingine ya huduma za jamii inayokidhi viwango vya kitaifa na kimataifa.
Ushiriki wa NHC katika maonesho haya unaakisi dhamira ya Shirika ya kuendelea kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali katika kujenga miundombinu imara inayochangia utoaji wa huduma bora za afya na maendeleo endelevu ya Taifa.
**NHC – Tunajenga Taifa Letu.**

πŸ—οΈ NAIBU WAZIRI MMUYA ATEMBELEA MRADI WA MAGHALA YA MTWARANaibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kas...
13/07/2026

πŸ—οΈ NAIBU WAZIRI MMUYA ATEMBELEA MRADI WA MAGHALA YA MTWARA
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kasper Mmuya, ametembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa Mradi wa Maghala ya Mtwara, unaotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika eneo la Viwandani, Manispaa ya Mtwara.
Mradi huu wa kimkakati unahusisha ujenzi wa maghala ya kisasa yenye uwezo wa kuhifadhi mazao kwa usalama, ikiwemo korosho, mbaazi, ufuta na mazao mengine ya biashara, hatua itakayochochea biashara, kuongeza thamani ya mazao na kuimarisha nafasi ya Mkoa wa Mtwara k**a kitovu muhimu cha biashara kupitia Bandari ya Mtwara.
Ujenzi wa mradi ulianza tarehe 5 Mei 2025 na unatarajiwa kukamilika 30 Septemba 2026, ukiwa na thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 4.1.
Ziara hiyo inaendelea kuonesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kusimamia utekelezaji wa miradi yenye tija inayochochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya wananchi.
TujengeTaifaLetu BuildingOurNation

πŸ“ Ubora haukadiriiwi... unapimwa.Wahandisi wa NHC wakiendelea na ukaguzi wa vipimo katika Mradi wa Tabora Commercial Com...
12/07/2026

πŸ“ Ubora haukadiriiwi... unapimwa.

Wahandisi wa NHC wakiendelea na ukaguzi wa vipimo katika Mradi wa Tabora Commercial Complex, kuhakikisha kila kazi inatekelezwa kwa usahihi na viwango vya kitaalamu.

Kila kipimo ni ahadi ya ubora. πŸ—οΈ

12/07/2026

Unalifahamu Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)?
Je, unajua nafasi yake katika kujenga Tanzania ya kisasa?
Shirika la Nyumba la Taifa lina jukumu la kujenga nyumba za makazi na majengo ya biashara kwa ajili ya kuuza na kupangisha, ili kuwawezesha Watanzania kupata makazi bora na mazingira rafiki ya kuishi, kufanya biashara na kuwekeza.
Mbali na hilo, NHC hutekeleza miradi ya ujenzi kwa kuzingatia mipango ya maendeleo iliyoidhinishwa na Serikali, hivyo kuchangia ukuaji wa miji ya kisasa, kuboresha mandhari ya maeneo mbalimbali na kuongeza thamani ya ardhi nchini.
Vilevile, Shirika linawezesha uzalishaji na upatikanaji wa vifaa vya ujenzi kupitia uwekezaji wake, hatua inayochochea ukuaji wa sekta ya ujenzi na maendeleo ya uchumi wa Taifa.
Lakini hayo siyo yote.
NHC pia huingia ubia na wawekezaji katika kuendeleza ardhi na kujenga miradi mikubwa ya makazi, biashara na matumizi mchanganyiko, pamoja na kusimamia mali zake ili ziendelee kutoa thamani kwa Taifa na wananchi.
Shirika la Nyumba la Taifa – Tunajenga Taifa Letu. πŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ—οΈ

🏑 JE, UMEPITA BANDA LA NHC SABASABA?K**a bado, leo ndiyo siku yako! Karibu upate taarifa sahihi kutoka kwa wataalamu wet...
12/07/2026

🏑 JE, UMEPITA BANDA LA NHC SABASABA?

K**a bado, leo ndiyo siku yako! Karibu upate taarifa sahihi kutoka kwa wataalamu wetu na ugundue fursa zinazoweza kubadilisha maisha yako.

Katika banda la NHC utapata maelezo kuhusu:
🏠 Nyumba za makazi na biashara za kupanga
πŸ”‘ Fursa za kununua nyumba za kisasa
πŸ—οΈ Miradi ya ubia na uwekezaji
πŸ‘· Huduma za ukandarasi na maendeleo ya miradi

Na k**a hutafanikiwa kutufikia Sabasaba, usiwe na wasiwasi. NHC ipo karibu nawe kupitia ofisi zetu zilizopo katika mikoa mbalimbali nchini, tayari kukuhudumia kwa weledi na kukupa mwongozo wa hatua kwa hatua.

Usikubali fursa ipite. Karibu NHC ujionee, uulize, ujifunze na uchague suluhisho linalokufaa.

NHC – Tunajenga Taifa Letu. πŸ‡ΉπŸ‡Ώ

RealEstate TujengeTaifaLetu

12/07/2026

Karibu Banda la NHC Sabasaba 2026 – Fursa za Makazi na Uwekezaji Zinakusubiri!
Jina langu ni Tobias Kavishe, Afisa Mauzo na Masoko wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).
Katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, NHC imekuja kuwakaribisha Watanzania kupata taarifa na huduma mbalimbali zinazotolewa na Shirika.
Katika banda letu utapata fursa ya kufahamu kwa kina miradi mbalimbali ya NHC inayotekelezwa nchini. Kwa upande wa Dar es Salaam tunayo Kijichi Residence pamoja na Kawe 711. Jijini Dodoma tunayo miradi ya Iyumbu Urban, Njedengwa na Medeli. Aidha, tunaendelea na utekelezaji wa miradi katika mikoa mingine ikiwemo Meru Business Park mkoani Arusha, Mkwakwani Plaza mkoani Tanga na Uluguru Plaza mkoani Morogoro.
Vilevile, banda la NHC limekusanya wataalamu kutoka idara mbalimbali ili kukuhudumia kwa karibu. Utapata taarifa kuhusu ununuzi wa nyumba, upangishaji wa nyumba na majengo ya NHC, fursa za uwekezaji kupitia miradi ya ubia (Joint Venture), pamoja na huduma nyingine zote zinazotolewa na Shirika.
Tunawakaribisha wananchi wote kutembelea banda letu. Ukiingia kupitia lango kuu la maonesho, elekea kwenye roundabout, kisha geukia upande wa kushoto kuelekea Barabara ya Biashara. Banda la NHC linapatikana upande wa kulia wa barabara hiyo.
Usikose fursa hii. Tunakuhudumia hadi tarehe 13 Julai. Karibu ujifunze, upate ushauri wa kitaalamu na ugundue fursa za makazi na uwekezaji zinazokufaa.
Shirika la Nyumba la Taifa – Tunajenga Taifa Letu.

πŸŒ… SAMIA HOUSING KIJICHI KUMEKUCHA! πŸ—οΈβœ¨Kila asubuhi inaleta hatua mpya. Kila hatua inaleta ndoto karibu zaidi kutimia.Sam...
11/07/2026

πŸŒ… SAMIA HOUSING KIJICHI KUMEKUCHA! πŸ—οΈβœ¨
Kila asubuhi inaleta hatua mpya. Kila hatua inaleta ndoto karibu zaidi kutimia.
Samia Housing Kijichi inaendelea kupaa, ikijenga zaidi ya nyumbaβ€”ikijenga maisha, fursa na kesho bora.
🏑 Hii si ndoto ya kesho, ni uwekezaji unaojengwa leo.
πŸ“ž Wasiliana nasi kupitia +255 684 445 004 ujipatie taarifa za kumiliki nyumba yako.

🏑 SABASABA BADO INAENDELEA!Zimebaki siku mbili pekee za Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasa...
11/07/2026

🏑 SABASABA BADO INAENDELEA!
Zimebaki siku mbili pekee za Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), na wananchi wanaendelea kutembelea banda la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kujionea fursa mbalimbali za makazi na uwekezaji.
Katika banda letu utapata maelezo ya kina kuhusu: 🏠 Upangishaji wa nyumba πŸ”‘ Ununuzi wa nyumba πŸ—οΈ Miradi ya ubia na fursa za uwekezaji
Usikose nafasi hii! Tembelea banda la NHC lililopo Mtaa wa Biashara ndani ya Viwanja vya Maonesho ya Sabasaba, upate ushauri wa kitaalamu na ujionee fursa zinazoweza kubadili maisha yako.
NHC – Tunajenga Taifa Letu. πŸ‡ΉπŸ‡Ώ

🏑 Je, ndoto yako ni kumiliki nyumba ya NHC?Au ungependa kujua utaratibu wa kupata nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa?K...
10/07/2026

🏑 Je, ndoto yako ni kumiliki nyumba ya NHC?

Au ungependa kujua utaratibu wa kupata nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa?

Karibu Banda Na. 77, Mtaa wa Biashara, Maonyesho ya Sabasaba (Kilwa Road, Dar es Salaam), upate:

βœ… Taarifa za miradi ya NHC iliyopo na inayokuja
βœ… Utaratibu wa kununua au kumiliki nyumba
βœ… Fursa za uwekezaji kwenye miradi ya NHC
βœ… Elimu kuhusu huduma zote zinazotolewa na Shirika

πŸ’¬ Tuambie kwenye maoni: Ukipewa nafasi leo, ungependa kumiliki nyumba ya NHC katika mkoa gani na kwa nini?

πŸ“ Tunakusubiri Banda Na. 77 – Mtaa wa Biashara.

NHC TEMEKE YAENDELEA KUCHOCHEA UWEKEZAJI WA VIWANDA NA BIASHARAAfisa Miliki Mwandamizi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NH...
10/07/2026

NHC TEMEKE YAENDELEA KUCHOCHEA UWEKEZAJI WA VIWANDA NA BIASHARA
Afisa Miliki Mwandamizi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Mkoa wa Temeke, Bw. Danstani Mgouya, amesema NHC imeendelea kuwa mdau muhimu katika kukuza uchumi kupitia uwekezaji katika sekta ya viwanda na biashara.
Ameeleza kuwa NHC Temeke inasimamia jumla ya majengo 267 ya biashara, ambapo sehemu kubwa ni maghala ya kisasa yanayotumika kuhifadhi bidhaa, mizigo na malighafi zinazohitajika na viwanda mbalimbali. Mkoa wa Temeke ni kitovu cha shughuli nyingi za viwanda, ukiwa na viwanda vinavyozalisha bidhaa za plastiki, vifaa vya ujenzi, rangi pamoja na vifaa vya ofisi.
Aidha, Bw. Mgouya amewahimiza wapangaji wa nyumba na majengo ya Shirika kulipa kodi kwa wakati, akisisitiza kuwa mapato ya kodi ndiyo msingi wa uwekezaji wa NHC. Amesema kupitia mapato hayo, Shirika linaendelea kuendeleza miradi mipya, kuboresha huduma kwa wateja na kuchangia ukuaji wa uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla.
"Unapolipa kodi kwa wakati, unachangia maendeleo ya Taifa kupitia uwekezaji endelevu wa NHC," alisisitiza Bw. Mgouya.

Address

P. O Box 2977
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 08:30 - 16:00
Tuesday 08:30 - 16:00
Wednesday 08:30 - 16:00
Thursday 08:30 - 16:00
Friday 08:30 - 16:00

Telephone

+255222105002

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when National Housing Corporation posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share