28/04/2025
NAWEZA KUJENGA NYUMBA KWA MILION 2 NA NIKAHAMIA?
Nimekutana na maswali je kweli kwa mil 2 naweza kujenga nyumba na nikahamia??
Jibu langu ni ndio unaweza kujenga na kuhamia au kumpangishia mtu akaishi hapo wakati wewe ukijipanga kujenga nyumba kubwa zaidi au kuhamia mwenyewe hapo ili kukwepa kodi sehemu ile uliyopanga.
Hapa chini ninakuwekea makadirio machache ambayo ukiyatumia vizuri basi utaweza kuwa na kajumba kako kakiwa na room mbili tu ya kuanzia maisha halafu baadae Mungu akikubariki basi utajenga kubwa zaidi.Sio lazima nyumba ikiwa na madoido mengi,finishing nyingi ndio iitwe nyumba,hata ikiwa haina rangi ni nyumbani kwako tambua kuna kale kafeeling kanakujaga unaporudi kwako na akili ikakuambia hapa ni kwako na sio umepanga kafeeling katamu sanaaa.
Mahesabu haya ya vyumba viwili inakuwa na;
1. Chumba kimoja single
2. Sebule ambayo imeungana na jiko hapohapo unapikia sebuleni ili mgeni ashikwe njaa mapema kwa kusikia harufu ya madikodikoπ
3. Choo cha jumuia au public toilet.
Kwahiyo kwenye kiwanja chako cha skwea mita 400 (20*20) unaweza kutangulia kujenga nyumba hii ndogo ukaishi hapo huku ukijipanga kujenga kubwa zaidi hapo baadae na kukwepa kulipa kodi kwa watu wengine basi ile kodi utaitumia kusave ili uje ujenge nyumba kubwa.
MATERIALS YA NYUMBA ROOM MBILI.:
1. Matofali brock 700 sawa na 1@ 900x700=630,000
2. Mchanga trip 2 sawa na 1@60000Γ2=120000
3. Siment mifuko 18 sawa na 1@15500Γ18=279000
4. Nondo mm12 ziwe 4 tu ambazo zinalazwa juu ya lenta kwa kubana mbilimbili sawa na 1@19000Γ4=76000
5. Kokoto trip 1 gari ndogo sawa na 60000
6. Mvao za kukodi za sahani pic 10 sawa na 20,000
7. Misumari kg 1 sawa 3500
8. Maji ya kujengea 30,000
9. Mbao za kuezeka
-2x4 idadi pic 5@4000x5 =20000
-mbao 2x3 idadi 4=1@3000Γ4=12000
- Misumari ya mbao kg 2 sawa 7000
- Misumari ya bati kg 2 sawa 7000
- bati simba dum nyeupe 16 pic bati zinaezekwa kwa kulazwa tu kuelekea nyuma ya nyumba sawa na 1@17500Γ16=245000
-grill madirisha 2 na kuweka geti moja mlango wa mbele 300,000
- mlango mmoja wa chumbani 200,000
-simenti za plasta ndani na sakafu 160,000 mifuko 10.
Hapo sasa jumla kuu Tsh 2,170,000.
Ufundi kuanzia mwanzo hadi mwisho tsh 600,000 kuanzia kujenga msingi,kupaua,kufix madirisha milango na kupiga plasta pamoja na sakafu rough floor tu.
Hapo jumla kamili tsh 2,770,000 tu.
Gharama hizi zinatofautiana bei sehemu moja na nyingine pia zinatofautiana katika namna ya usafirishaji,lakini hadi kufikia hapo itakuwa tayari kukaliwa hata ukihitaji kuhamia ni sawa huku vitu vingine vidogo vidogo vikifanyika ukiwa kwako.
Sio lazima kufanya finishing za kibabe k**a tailizi,rangi nk kwasababu hii ni nyumba ya dharula unaishi hapo ukijipanga kujenga kubwa zaidi na pale ukimaliza ujenzi wa nyumba kubwa hii ndogo utaifanyia finishing unazotaka na kuipangisha au kutumia kwa mahitaj mengine.
Natumain hadi hapa naweza kuwa nimeeleweka hizi gharama zinapanda na kushuka hazifanani kila eneo.
Nimekwepa kufunga nondo chini kwasababu hii nyumba ni ya dharula tu badala yake nikafunga lenta ya juu ili madirishani na milangoni kusiweke nyufa mapema.
K**a mtu ana swali tafadhali nione whatsap kwa ufafanuzi zaidi 0689906466 mashauriano ni bure kabisa.
Imeandikwa na Eng. Kennedy Cornely
Haya wadau kazi ni kwenu,nitaendelea kuwaletea makala k**a hizi pengine zitamsaidia mtu mmoja kufanya jambo si eti?
Kumbuka kuanzia 200,000/= tu unaweza kumiliki kiwanja Bagamoyo Masuguru
Marm'z Relationship Hub Marm'z Real Estate 0710474782