Farnes Zone

Farnes Zone 🌍 Farnes Zonne – Chanzo chako cha habari, mitindo, biashara, elimu, matangazo na motisha.

Tunakuunganisha na ulimwengu wa maarifa, ubunifu na mafanikio kila siku.

Mmoja wa magwiji wakubwa wa soka atahitimisha taaluma yake bila kushinda taji muhimu zaidi, baada ya mechi ya mwisho ya ...
13/07/2026

Mmoja wa magwiji wakubwa wa soka atahitimisha taaluma yake bila kushinda taji muhimu zaidi, baada ya mechi ya mwisho ya Kombe la Dunia ya Cristiano Ronaldo akiwa na Ureno kumalizika kwa kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Uhispania katika hatua ya 16 bora.

Mchezaji huyo alibubujikwa na machozi wakati safari yake ya Kombe la Dunia ilipofikia tamati, kufuatia bao la ushindi lililofungwa na Mikel Merino katika muda wa nyongeza, bao lililoiwezesha timu ya nchi jirani kusonga mbele.

Akiwa na umri wa miaka 41, mchezaji huyo ambaye ameshinda tuzo ya Ballon d'Or mara tano, Ligi ya Mabingwa mara tano na Kombe la Mataifa ya Ulaya (Euro) mwaka 2016, amefunga mabao 976 —rekodi ya dunia— akiwa na klabu zake pamoja na timu ya taifa.

Amefunga mabao katika mashindano sita ya Kombe la Dunia, rekodi ya kihistoria.

Hata hivyo, hatua ya karibu zaidi aliyofikia katika mbio zake a kushinda Kombe la Dunia ilikuwa mwaka 2006, wakati Ureno ilipotinga nusu fainali.

Tayari alikuwa ametangaza kuwa hili lingekuwa Kombe lake la Dunia la mwisho, lakini baada ya mechi hiyo alisema: "Nitajadiliana na familia yangu na kufanya maamuzi kwa utulivu," alipoulizwa iwapo ataendelea kuichezea timu yake ya taifa.

Skip content and continue reading

'Nadhani mimi ni mchezaji niliyekamilika zaidi kuwahi kutokea' - Ronaldo7 Februari 2025

Ronaldo na Messi - Ushindani ambao ulitawala soka kwa miongo miwili - lakini nani bora zaidi kati yao?10 Juni 2026

End of content

Mjadala utaendelea kuwa wazi laitiUreno wangekuwa na nafasi nzuri zaidi ya kushinda Kombe hili la Dunia bila shinikizo la kumwanzisha Ronaldo - mchezaji wa klabu ya Al-Nassr - katika kila mechi.

25/10/2025

Karibu kwenye matangazo ya moja kwa moja ya FARNES TV, sauti ya matumaini na mabadiliko! Tazama mahojiano, muziki, mijadala ya jamii, na simulizi halisi kutoka kwa watu wanaoleta nuru katika dunia. Hapa tunaguswa, tunajifunza, na tunainua jamii kupitia ukweli na imani. đź’«
👉 Jiunge nasi sasa — usipitwe na sauti ya kizazi kipya!
Hashtags:

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) nchini Tanzania imetangaza kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, utakaohusisha nafasi ...
24/10/2025

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) nchini Tanzania imetangaza kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, utakaohusisha nafasi ya Rais, wabunge na madiwani, utafanyika siku ya Jumatano, tarehe 29 Oktoba 2025.

Akizungumza katika uzinduzi wa ratiba ya uchaguzi huo jijini Dodoma leo, Mwenyekiti wa INEC, Jaji wa rufaa Jacob Mwambegele, amesema maandalizi ya uchaguzi huo yameanza rasmi na kuainisha tarehe muhimu katika kalenda ya uchaguzi.

Kwa mujibu wa Jaji Mwambegele, utoaji wa fomu za uteuzi kwa wagombea wa nafasi ya Rais na Makamu wa Rais utafanyika kati ya Agosti 9 hadi 27, 2025. Aidha, ameongeza; "Tarehe 27 Agosti 2025 itakuwa siku ya uteuzi wa wagombea wa kiti cha rais na makamu rais, uteuzi wa wagombea ubunge na uteuzi wa wagombea udiwani", alisema Jaji huyo.

Kwa upande wa kampeni, Tanzania Bara itakuwa na kipindi cha kampeni kuanzia Agosti 28 hadi Oktoba 28, huku Tanzania Zanzibar kampeni zikiendeshwa kuanzia Agosti 28 hadi Oktoba 27, ili kupisha upigaji wa kura ya mapema.

"Tarehe 29 Oktoba, 2025 siku ya Jumatano itakuwa ndio siku ya kupiga kura", alisema Mwambegele, kuhusu uchaguzi huo unaolenga kuwapa wananchi fursa ya kidemokrasia kuchagua viongozi wao wa ngazi mbalimbali.

Nilipofika kwenye mgahawa wa TAMUTAMU uliopo katikati ya mji wa Nairobi Kenya mapema asubuhi, nilikutana na mmiliki wa M...
24/10/2025

Nilipofika kwenye mgahawa wa TAMUTAMU uliopo katikati ya mji wa Nairobi Kenya mapema asubuhi, nilikutana na mmiliki wa Mgahawa huo Sam Nkya akiwa katika pilikapilika za maandalizi ya chakula cha mchana.

"Jamani tufanye chap chap (harakaharaka) wateja wa lunch (chakula cha mchana) huja mapema Alhamisi", Nkya aliwaeleza wafanyakazi wake katika mgahawa huu unaoandaa vyakula vya asili vinavyoliwa uswahili na asili ya pwani ya Afrika Mashariki.

''Nilipenda tu mapishi ya vyakula hivi vya Kiswahili. Mama aliopenda sana kutuandalia mapochopocho tukiwa watoto na nikatamani sana kuwa mpishi maarufu na kuamua kufanya biashara hii, kitu ambacho nakipenda sana,'' alisema Sam.

Japo angeendeleza ndoto yake nyumbani Dar es Salaam, Tanzania anawaandalia wateja wake katika migahawa kadhaa jijini Nairobi ambapo amepaita nyumbani kwa zaidi ya miaka mitano sasa.

Kwa pamoja na mke wake, wanakuza familia yao changa na kujitafutia Riziki ya kila siku mbali na nyumbani kwao Sam ambaye anasema siku moja angependa kurejea na kupanua biashara yake huko na labda kuwapa Watoto wao nafasi ya kuijuwa Tanzania k**a anavyoifahamu yeye.

Jumuiya ya wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA) nchini Tanzania imetoa tamko la kusikitishwa kwakwe na ma...
23/10/2025

Jumuiya ya wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA) nchini Tanzania imetoa tamko la kusikitishwa kwakwe na matukio ya watu kupotea au kudaiwa kutekwa, kikisema hali hiyo inatishia uhuru wa kujieleza na misingi ya haki za binadamu nchini.

Katika taarifa yake, UDASA imesema matukio hayo yamezua hofu miongoni mwa wananchi na kuathiri taswira ya taifa katika jamii ya kimataifa.

Jumuiya hiyo imeitaka serikali na vyombo vya usalama kuchunguza kwa uwazi na kwa haraka visa vyote vya aina hiyo ili kutoa majibu ya kweli kwa umma.

Tamko hilo limerejea ripoti ya shirika la haki za binadamu (LHRC) kuhusu tishio la kile kinachoidwa "Watu wasiojulijkana" wakilitupia lawama Jehsi la Polisi kwa ama kushindwa kudhibiti au kutolea ufafanuzi.

Hata hiyo mara kadhaa Jeshi la Polisi limeeleza kuendelea kufuatilia wanaodaiwa kutekwa, na lilishawahi kukanusha kutohusika na wapo wengine waliodaiwa kutekwa kubainika kujiteka.

23/10/2025

ZONE đź’« ni jukwaa la ubunifu, maendeleo na nafasi za fursa kwa vijana na jamii. Tunasimama k**a daraja kati ya talanta, elimu, ajira, ujasiriamali na ubunifu kwa lengo la kuinua maisha ya watu kupitia miradi yenye matokeo halisi.

Kupitia matawi yetu mbalimbali k**a FARNES EDUCATION, FARNES CUP, FARNES OPPORTUNITY na program nyingine maalum, tunatoa mazingira rafiki ya kujifunza, kugundua uwezo, kukuza vipaji na kujenga kizazi chenye uthubutu wa kufanikiwa.

Katika FARNES ZONE 💫 tunaamini kuwa kila mtu ana nafasi yake ya kung’aa, na jukumu letu ni kufungua mlango wa fursa hizo kwa njia ya kidigitali, kijamii, na kiubunifu.

Marekani imetangaza vikwazo vipya vinavyolenga makampuni mawili makubwa zaidi ya mafuta nchini Urusi - Rosneft na Lukoil...
23/10/2025

Marekani imetangaza vikwazo vipya vinavyolenga makampuni mawili makubwa zaidi ya mafuta nchini Urusi - Rosneft na Lukoil - katika juhudi za kuishinikiza Moscow kufanya mazungumzo ya makubaliano ya amani nchini Ukraine.

"Kila wakati ninapozungumza na Vladimir, ninakuwa na mazungumzo mazuri na kisha hawaendi popote," Rais Donald Trump alisema, baada ya mkutano na Katibu Mkuu wa Nato Mark Rutte kujadili mazungumzo ya amani.

Tangazo la vikwazo hivyo limekuja siku moja baada ya Trump kusema kuwa mkutano uliopangwa kufanyika na Rais wa Urusi Vladimir Putin mjini Budapest utasitishwa kwa muda usiojulikana.

Mapema Jumatano, Urusi ilitekeleza mashambulizi makali ya mabomu dhidi ya Ukraine yaliyoua takriban watu saba wakiwemo watoto.

Polisi nchini Uganda wanasema watu arobaini na sita wamefariki katika ajali ya barabarani iliyohusisha magari manne kand...
23/10/2025

Polisi nchini Uganda wanasema watu arobaini na sita wamefariki katika ajali ya barabarani iliyohusisha magari manne kando ya Barabara Kuu ya Kampala-Gulu 46, kufuatia taarifa mpya kutoka kwa maafisa wa hospitali.

Maafisa wanasema baadhi ya waathiriwa waliodhaniwa kuwa wamekufa hapo awali walipatikana wakiwa wamezira na sasa wanapokea matibabu.

Wafanya kazi wa kutoa huduma za dharura wanashirikiana na maafisa wa afya kuthibitisha idadi hiyo na kutoa taarifa sahihi huku uchunguzi ukiendelea kubaini chanzo cha mkasa huo.

Ajali hiyo iliyotokea Jumatano asubuhi,katika Kijiji cha Kitaleba, ilihusisha mabasi mawili, Lori na Gari ndogo aina ya Toyota Land Cruiser, kwa mujibu wa ripoti ya awali ya polisi.

Idadi ya vifo inatarajiwa kuongezeka kutokana na baadhi ya abiria kujeruhiwa vibaya.

“Inaelezwa kuwa basi lililokuwa likitoka Kampala lilikuwa likilipita lori na basi jingine lililokuwa likielekea Kampala lilikuwa likiipita gari ndogo ya Toyota Land Cruiser, lakini lilishindwa kufanya hivyo kwani tayari basi lililokuwa likitoka Kampala lilikuwa limekaribia’’. Taarifa ya polisi imeeleza.

Mahak**a Kuu ya Umoja wa Mataifa imesema Israel imeshindwa kutimiza wajibu wake wa kibinadamu huko Gaza.Mahak**a hiyo im...
22/10/2025

Mahak**a Kuu ya Umoja wa Mataifa imesema Israel imeshindwa kutimiza wajibu wake wa kibinadamu huko Gaza.

Mahak**a hiyo imesema kuwa Israel ilizuia misaada ya kibinadamu kuingia Gaza mara mbili.

Mahak**a hiyo inaamini kwamba "uhamishaji wa kulazimishwa wa wakaazi wa maeneo yanayokaliwa kimabavu ni jambo lisiloruhusiwa" na ni lazima lisitishwe.

Address

Nyarugusu Camp
Kasulu
74401

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Farnes Zone posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category