29/03/2025
JE UMAARUFU NA KUWA NA PESA NYINGI NDO HATIMA??
Kuwa mtu maarufu, au mwenye pesa sio hatima.. Wala maono.
Kuna watu wengi leo wanalia kwa sababu tamaa yao ilikuwa ni pesa, na kweli wakazipata, lakini walipoteza hatima zaoo.. wakabaki kulia na kujutia, kwanini wana pesa na maisha Yana huzuni? Kwanini wana pesa lakini amani haipo? Kwanini wana vitu tele na anaweza kwenda atakako lakini bado, maisha yake ni utumwa na mateso..
Watu wengi huwahisha hatima zao kwa tamaa ya pesa, Hasa vijana wengi Sana, kwa sababu hatima usipoilinda na kuitunza, kwa kudhihirisha kwa ulimwengu kwamba unayo inabaki ndani yako, mpaka atokee mtu wa kukusaidia.. ndio maana watu wengi wamekufa na hatima kubwa Sana za utajiri udumuo na heshima.
Kundi kubwa wanaamini, ukiwa na pesa tu basi ndo Kila kitu, ndio maana utamkuta mhubiri mzuri Sana, ukiangalia ana kusudi la kuhubiri injili ya kweli kimataifa, lakini kwa tamaa ya pesa anadanganyika, anapotoka kwa miujiza feki, uongo na utapeli..baada ya ..miaka kapotea, bila heshima.
Kundi la wasanii vilevile wanadanganyika mtu ni mwimbaji mzuri ukiangalia huyu atafika mbali lakini kwa tamaa ya pesa anaingia kwenye kutaka pesa za chapu, mikataba freemason, kwa waganga.. .kweli wanampa madawa ya masharti anavuma na kutamba na vipesa na magari ya kifahari baada ya muda amepotea
Nikukumbushe watu walioishi hatima zao, Ev. Kulola, Baba Lola, Bonke, Kenneth hageni, Benson Idahosa, wasanii Remi ongala, na wengine wengi...unaona wamedumu katika hatima zao, zimewaletea utajiri na heshima.
Haina maana pesa ni mbaya Ila tafuta pesa ndani ya kusudi la kuletwa kwako duniani, unaupata utajiri wenye heshima na utukufu kwa Mungu.