07/07/2021
Namshukuru sana Mungu kwa kunileta Duniani Siku na tareh k**a ya leo Leo nisiku yangu ya kumbukizi ya kuzaliwa huwaga naitumia Siku hii kwakupumzika na kufurahi k**a ilivyo andikwa kwenye maandiko matakatifu yakuwa Mungu alipumzika katika uumbaji wake Siku ya Saba ni Siku ya sabato Saba ni utimilifu sasa hapa kwangu zipo mbili yaan (double) 7,7, means you get it double double blessings okey Nina makala Moja juu inayohusu
Hauwezi kulitatua tatizo kwa KULIKIMBIA.
Ni kweli ni jambo gumu sana sana...
..ila haliwezi kuisha kwa kulikwepa.
Umeshawahi kuwa kwenye changamoto ambayo unatamani K**a ungetokea muujiza tu IKAYEYUKA?
Au unatamani hata ungepotea tu kinamna na ujikute hauko tena hapo ulipo?
Wewe sio wa kwanza kuna wengi walishawahi kupitia hali hii.
Inaweza kuwa ni changamoto kwenye...
..mahusiano yako.
..inaweza kuwa ni jambo lililopo kazini n.k
Mara nyingi mtu akipitia hali hii huwa anataka...
..KUKIMBIA.
..KUJIFICHA.
..na APOTEE KABISA.
Unachotakiwa kujua ni kuwa, njia rahisi ya kushughulika na changamoto yako ni KUIKABILI.
Kwa sasa inaonekana k**a hauna Nguvu na ukiikabili ndio itakuwa mwisho wako.
SIO KWELI!
Aibu unayoiogopa hautaipata k**a ukiikabili badala ya kuikimbia.
Hasara unayoihofia haitakuwepo k**a utaamua kuikabili.
Hii changamoto Leo.
Leo nakuombea uchukue HATUA YA KWANZA kuikabili changamoto YAKO...
..na utaona Mungu atakavyokupa USHINDI.
Niimani yangu umepata kitu..
See You At The Top