01/02/2022
Kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi, Dunia inakabiliwa na janga la njaa katika maeneo mbalimbali. Vyanzo vya Maji hasa mito na chemchem zimepungua ujazo wa Maji Kwa kiwango kikubwa sana.
MKULIMA AFANYE NINI?
1. Kuwa makini kwenye uchaguzi wa maeneo ya kilimo hasa yenye uwezekano wa kupata Maji ya kuchimba ardhini.
2. Otesha miti ya kutosha katika eneo lako, hasa ya matunda Kwa kuwa miaka ijayo matunda yanaweza kuwa biashara nzuri na pia inatunza mazingira
3. Fuatilia vyombo vya habari, mamlaka za hali ya hewa na tabia nchi pamoja na chakula. Itakusaidia kufanya uamuzi sahihi katika kazi zako
4. Usiache mzigo unaokupa faida mpaka ukose soko. Mfano, mahindi kwa sasa gunia ni zaidi ya elfu 75 Arusha, na wakati wa mavuno ilikuwa Hadi elfu 30 gunia. Kusubiri faida kubwa sana kunaweza kukuponza au ikakupa faida. Shika unachokiona kabla hakijaondoka.
Kwa mifugo vivyohivyo, mfugo ukifika hatua inayofaa kuvuna basi vuna usisubiri mpaka upate hasara ya kumlisha au kufa Kwa mfugo wenyewe.
5. Jijengee kusoma mbinu za kufanya shughuli zako kitaalamu hata k**a ni mtalamu, mambo yanabadilika
6. Fanya mambo yako Kwa mrengo wa kibiashara. Kila hatua au shughuli unayoifanya weka kumbukumbu ya gharama ili ujue faida. Si vema kupoteza muda na fedha pasipo kujua.
7. Fuata Sheria za nchi hasa zinazohusu shughuli zako. Usitume kemikali zisizoruhusiwa kuhifadhia mazao, itakuharibia sifa.
8. Tembelea watu wanaojihusisha na unachojihusosha nacho. Utajifunza na kuboresha kwako Kwa kubadilishana mawazo na taarifa za masoko pia
9. Fanya utafiti juu ya faida na changamoto za shughuli unayoitarajia kuanzisha. Itakusaidia kupima k**a una uwezo wa kuvumilia changamoto hizo Kwa faida utakazojifunza
10. Weka jitihada katika kuboresha shughuli zako na kutafuta masoko