12/08/2025
NENO DALALI TUMEKOPA INDIA
Neno DALALI asili yake ni lugha ya Kihindi,sisi kwa Kiswahili tumetohoa,k**a tulivyotohoa maneno mengine mengi kutoka lugha zingine,kwa mfano neno kamisheni (Commission) tumelitohoa kutoka lugha ya kiingereza.Tafsiri ya neno DALALI katika lugha ya kihindi ni mtu anayetoa huduma ya kushauri na kuwaunganisha mnunuzi na muuzaji wa mali,k**a vile kiwanja,nyumba au mali nyinginezo,au kuwakutanisha mwenye mwenye nyumba au jengo na mpangaji wa nyumba,au jengo lolote aidha kwa makazi au biashara kwa lengo la kupanga.
Baada ya kukamilika kwa huduma ya DALALI hupata stahiki ya malipo ya ada ya malipo ambayo kwa lugha ya kiingereza inajulikana k**a ‘commission’, ada hii ya huduma hupaswa kulipwa na aidha muuzaji au mnunuzi ama mpangishaji au mpangaji,ikitegemea ni nani kati ya hao alikuwa amempa kazi DALALI huyo.
Nchini India biashara ya udalali/wakala wa milki (Real Estate Agency),inaheshimika sana,na hii inatokana na kuwa mchango mkubwa katika ukuaji wa sekta ya milki kuu nchini humo,kwa vile shughuli hii inaratibiwa na serikali,kuna sheria,miongozo na mamlaka ya uratibu na usimamizi ijulikanayo k**a Real Estate Regulatory Authority (RERA).
Mamlaka hii inajukumu la kuwasajili madalali wa milki, kuwapa leseni na kuhakikisha madalali wa milki wanafanya kazi kwa weledi,uadilifu,uwazi na uaminifu,na ikitokea DALALI/WAKALA akakihuka misingi hii,mamlaka itamchukulia hatua za kinidhamu,ikiwemo kufungiwa leseni ya UDALALI/WAKALA kwa muda au Maisha kulingana na uzito wa kosa lililotendwa.
Na ikitokea umefungiwa leseni ya UDALALI/WAKALA na kwa makusudi bila kujali ukaendelea kufanya shughuli hii, ukikutwa na hatia kwa kosa hili unaweza kuhukumiwa adhabu ya kifungo na faini kubwa.
Kwa Tanzania,licha ya umuhimu wake mkubwa katika ukuaji wa sekta ya Ardhi,neno DALALI/WAKALA halina taswira nzuri kidogo, mbele ya baadhi ya wanajamii ,hasa hasa madalali wa milki kuu,wale kuuza au kununua Ardhi,na wale kupangisha nyumba au vyumba,hii haimaanishi hakuna MADALALI/WAKALA wenye maadili,la asha wapo MADALALI/WAKALA wengi sana,wanaofanya kazi zao kwa weledi na uaminifu mkubwa na wamewasaidia Watanzania wengi kutimiza ndoto zao, kwa kupata viwanja na nyumba nzuri za kununua,au kupanga.
Taswira ya UDALALI Tanzania shida sio neno lenyewe Dalali au udalali,la asha changamoto hapa ni mambo yasiyoridhishwa ambayo yamekuwa yanafanywa na baadhi ya Madalali wasiokuwa waaminifu na weledi,kushiriki katika kufanya vitendo vya udanganyifu na utapeli,na hivyo kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu,jambo ambalo ni kosa na kinyume cha sheria ya mwenendo wa makosa jinai,lakini pia wamekuwa wakichangia katika kuendelea migogoro ya Ardhi nchini.
Kwa sasa tasnia hii nchini,haina usimamizi wa mamlaka maalum,kwahiyo kwa kiwango kikubwa sana,inaendeshwa kiholela,na hivyo kutoa mwanya kwa wale wachahche wasiokuwa waaminifu,kuipaka matope na kuipa dosari kazi ya udalali nchini,na hii sio kwa sekta ya udalali tu,sekta yeyote ile ikikosa usimamizi wa karibu wa mamlaka,kupitia sheria,kanuni na miongozo,ni rahisi kujiingiza katika vitendo vyenye kuwaumiza wengine,mfano sekta ya usafirishaji,ikiachwa ijiendeshe kiholela,lazima tutashuhudia nauli kupanda kiholela,nyakati za asububi na jioni kwa dala dala,au kipindi cha likizo kwa mabasi ya mikoani,au madereva kubadilisha ruti walizopangiwa.
Vitendo vya udanganyifu na utapeli vinavyofanya na baadhi ya madalali wachache nchini, vinaweza kupungua kwa kiasi kikubwa,endapo kutakuwa mamlaka ya usimamizi na uratibu,na hivyo kuwajibishwa wale wachache ,pale tu wanapokiuka utaratibu.
Nchini marekeani ili mtu afanye ya kazi ya udalali/ wakala wa nyumba au viwanja,kupanga au kupangisha ni lazima apate leseni kutoka mamlaka za serikali,na ili upate leseni nu budi uwe na sifa stahiki,miongoni mwa sifa hizo;umri kuanzia miaka 18,elimu ya juu/diploma,kusoma na kuhitimu kozi za milki kuu,kufanya mitihani na kufaulu,uchunguzi wa historia (background check) hapa ikibainika ulikutwa na kosa na jinai na ukafungwa,hii ni rekodi yauhalifu upewi leseni,na ukilazimisha kufanya udalali/wakala bila kuwa na leseni adhabu yake ni kifungo na faini,hii pia inawahusu wale waliopewa leseni na kisha kukikuka masharti ya leseni,na kupelekea kufungiwa leseni hizo aidha kwa muda au Maisha,nao wakikaidi na kuendelea na kutoa huduma hii,watakutwa na adhabu hii.
Katika mazingira ya utaratibu wa namna hii,ukianzishwa nchini sio rahisi kusikia au kuona vitendo ya udanganyifu na utapeli vikiendelea katika sekta ya Ardhi na milki kuu,nadiriki kusema tumechelewa sana kutokuwa na sheria,kanunni,miongozo na mamlaka ya namna hii,nasema tumechelewa kwa sababu sekta ya udalali ni injini ya kubwa sana ya ukuaji wa uchumi wa taifa letu nitaeleza hapa,kiuchumi nyenzo za uzalishaji mali (factors of productions) zipo nne,nazo ni Ardhi (land),mtaji (capital),nguvukazi (labours) na entrepreneurship (ujasiliamali),ila ardhi ndiyo nyenzo kuu ya uzalishaji mali katika hizi nne,kwa sababu shughuli zote kibinadamu hufanyika juu yake,sasa katika hizi nyenzo nne,nyenzo mbili ni nyeti ambayo ni Ardhi na mtaji, kwa sababu nguvukazi ipo ya kutosha,ukitangaza ajira leo ,unahitaji mtu mmoja,wanaomba 1000,wajasiliamali tunao wa kutosha,wakubwa na wadogo lakini changamoto yao kubwa ni ardhi na mtaji.
Sasa ili kupunguza changamoto hii ya Ardhi na mtaji ni budi tuwe na soko la ardhi fanisi (efficient land markets),na hili kuwe na soko la ardhi fanisi,dalali hapo anaingia k**a kiunganisha muhimu kwa taarifa na maarifa kuwezesha mjasiliamali mwenye mtaji kupata ardhi sahihi, na mjasiliamali mwenye ardhi kupata mtaji kupitia kuuza ardhi yake,kwa vile ardhi ni mali na ni mtaji.
Pia sekta hii ikisimamiwa na mihamala ya milki kuu ikawa inarekodiwa itakuwa rahisi kwa serikali kupata kodi,na kuchangia katika pato taifa letu kwa kiwango kikubwa.
Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,chini mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ,imefanya juhudi kubwa sana, katika kuinua na kuboresha sekta ya Ardhi nchini,kupitia wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,k**a vile kuzindua sera ya Ardhi ya 1995 toleo la 2023,kuanzisha mfumo wa Ardhi kidigitali (https://eardhi.lands.go.tz),lakini pia kuazishwa kwa kitengo miliki ndani ya wizara hii,hivyo nina matumaini kuwa ile miswada ya milki kuu,na madalali/wakala,itakuwa sharia kamili na kuanzishwa kwa mamlaka hii,ambayo itakuwa na jukumu la kusimamia madalali na kuhakikisha wanafanya kazi kwa weledi na uaminifu,na kuchangia katika pato la taifa,pia kuhakikisha wanunuzi wa ardhi ,nyumba na majengo maslai yao yanalindwa.Kwa kufanya hivi tutaongeza kujiamini (confidence) kwa wadau wote wa sekta ya Ardhi,hii itaongeza ufanisi wa soko la Ardhi (efficient land markets),hii itaongeza tija na tunaweza kuona kwa mara ya kwanza ukuaji mkubwa wa sekta ya Ardhi katika kiwango cha kimataifa.
Imeandikwa na;
Fadhil M. Mkwachu
(Land Consultant)
FAAMMO REAL ESTATE-DODOMA
0712 222 258/0755 802 121