Magulumatali Yetu

Magulumatali Yetu Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Magulumatali Yetu, Real Estate, 65, Chalinze.

MAGULUMATALI  FC YAANZA MWAKA MPYA KIBABE, YAICHAPA MKENGE FC .Kusherehekea Sikukuu Ya Mwaka Mpya,  Leo Kumefanyika  Mec...
01/01/2024

MAGULUMATALI FC YAANZA MWAKA MPYA KIBABE, YAICHAPA MKENGE FC .

Kusherehekea Sikukuu Ya Mwaka Mpya, Leo Kumefanyika Mechi Ya Kirafiki Kati Ya Magulumatali Fc Dhidi ya Mkenge Fc, Mechi Iliyochezwa Katika Uwanja Wa Magulumatali

Mechi Hiyo Imemalizika Kwa Magulumatali Fc Kuibuka Na Ushindi Wa Goli Moja Kwa Bila, Goli Lililowekwa Kimiyani Na Mchezaji Selemani Pendo.

Pia Mechi Hiyo Imetumika K**a Maandalizi Ya Mashindano Ya Kombe La Jezi Linalotarajiwa Kutimua Vumbi Kuanzia Siku Ya Jumamosi Ya Tarehe 6 Ambapo Kwa Taarfa Za Awali Ni Kwamba Timu Zote Mbili Hizo Zitashiriki Mashindano Hayo.

Mechi Nyingine Ya Kirafiki Ilitarajiwa Kufanyika Katika Kiwanja Cha Shule Ya Msingi Talawanda Kati Ya Talawanda Fc Dhidi Ya Kiembe Fc, Lakini Mechi Hiyo Haikufanyika Huku Sababu Za Kutofanyika Kwake Kutowekwa Wazi.

NB :Pale Walipoishia Mwaka 2023 Ndipo Wanapopaendeleza Mwaka 2024😁

MWENYEKITI UVCCM ASIKITISHWA NA VIONGOZI  WASIOHUDHULIA VIKAO VYA CHAMA.Mwenyekiti Wa Jumuia Ya Vijana (UVCCM)   Wilaya ...
31/12/2023

MWENYEKITI UVCCM ASIKITISHWA NA VIONGOZI WASIOHUDHULIA VIKAO VYA CHAMA.

Mwenyekiti Wa Jumuia Ya Vijana (UVCCM) Wilaya Ya Bagamoyo, CDE. Hafidhi Nassoro Konyamale amesikitishwa na Baadhi ya Viongozi Wasiofika Katika Vikao Vya Mabaraza ya Chama Cha Mapinduzi .

Hayo Ameyasema Jana Wakati Akiongea Na Wajumbe Wa Baraza La Uvccm Wilaya ya Bagamoyo Wakati akiwa Katika Baraza La Uvccm Wilaya Ya Bagamoyo Lililofanyika Katika Viwanja Vya Shule ya Sekondari Kibindu, Kata Ya Kibindu Halmashauri ya Wilaya Chalinze.

"Binafsi Sijaridhishwa na Wajumbe Wa Baraza Ambao Hawakufika Katika Baraza Hili, Kwani Moja Ya Nguzo Imara Ya Chama na Viongozi Wake Ni Kushiriki Vikao Vya Jumuia Pamoja na Mabaraza Yake. Baraza Hili Lipo Kikanuni Ndani Ya Jumuia Yetu, Lengo Ni Kuangalia Mafanikio Ya Jumuia Katika Muhura Wa Pili Wa Mwaka Na Wapi Paboreshwe Ili Kuongeza Ufanisi Katika Jumuia Yetu ya Vijana Wilaya Ya Bagamoyo " Amesema

Mwenyekiti Huyo Ameongeza "Fikilia Kiongozi Hafiki Kwenye Kikao Cha Baraza, Je Tutajuaje Changamoto Anayokutana Nayo Tunapohitaji Taarfa Za Utekelezaji Ndani Ya Eneo Lake?? Kiufupi ni Kitu Kisichoridhisha Kwani Viongozi K**a Hawa Ndio Wataokwamisha Ilani Ya Chama Katika Kutekeleza Ilani Yake "

Pia Mwenyekiti Huyo Ameelezea Mikakati Ya Jumuia Hiyo kuelekea Uchaguzi Mdogo Wa Diwani Katika Kata Ya Fukayosi Utaofanyika Mwezi February Kufuatia Kifo Cha Aliyekua Diwani Wa Kata Hiyo Ally Ally Aliyefariki Dunia Siku Za Karibuni. Hivyo K**a Wanajumuia, Wanatakiwa Kuhakikisha Kua Chama Chao Kinarudi Katika Kiti Cha Kuiongoza Kata Hiyo.

CDE Konyamale Amezitaja Baadhi Ya Kata Zilizoonesha Uhafifu Wa Ushiriki Katika Baraza Hilo Kua Ni Kata Ya Kiwangwa, Ubena, Vigwaza, Fukayosi Huku Kata Ya Msata Ikiwakilishwa na Mwenyekiti, Katibu Pamoja Na Katibu Hamasa Pekee. Wakati Huo Huo Kata Ya Talawanda Pamoja na Pera Zikiwa Na Idadi Nzuri Ya Viongozi Walioshiriki Baraza Hilo .

Jana Jumuia Ya Vijana Wilaya ya Bagamoyo Imefanya Kikao Cha Pili Cha Baraza Kwa Mwaka 2023 Ambalo Lipo Kikanuni Katika Kata Ya Kibindu Halmashauri ya Wilaya Chalinze Ambapo Kabla Ya Kufanyika Kwa Baraza Hilo,Aliweza Kutembelea Kituo Cha Afya Kibindu Pamoja Na Kupanda Miti, Kutembelea Soko La Kibindu Na Baadae Kufanya Mkutano Wa Hadhara Na Wanakijiji wa Kata Ya Kibindu.

Uvccm Magomeni Bagamoyo
UVCCM Bagamoyo
Uvccm Mapinga
Uvccm Kata Ya Talawanda
Uvccm Kata Ya Msata
Uvccm Kata Ya Kiwangwa


Binafsi Sio Mtu Ninaepingana na Mila Na Tamaduni Za Kabila Letu La Wakwele Kwani Najua Katika Vitabu Vimeorodhesha Faida...
31/12/2023

Binafsi Sio Mtu Ninaepingana na Mila Na Tamaduni Za Kabila Letu La Wakwele Kwani Najua Katika Vitabu Vimeorodhesha Faida Mbalimbali Za Kuendeleza Mila Kwa Jamii Husika Na Taifa Kwa Ujumla.

Lakini Nitakua Kinyume Na Aina Ya Matukio Na Gharama Kubwa Za Utekelezaji Wa Hizi Mila, Hali Inayopelekea Baadhi Ya Watu Nje Ya Jambo Husika Kukosa Kufanya/Kufanyiwa Jambo La Msingi Kutokana Na Utekelezaji Wa Hizi Mila

Mfano, Gaharama Ndogo Ya Kuandaa Ngoma Kwa Mtoto Hadi Kumalizika Haipungui 1 Million. Ukiangalia Kipato Cha Mhusika Hakimshawishi Kufanya Jambo Husika, But The Way Anavyopambana Kuhakikisha Sherehe Kufanyika Unaona Kabisa Kuna Kitu Anakitafuta.

Then Kuna Wale Wanatumia 1 Million Plus Kugharamikia Ngoma Ila Baada Ya Mwezi Mmoja Mtoto Wake Anafaulu Kwenda Chuo Au Shule Akaendeleze Elimu, Anaambiwa Baki Home Hatuna Hela, Aiseeh Ni Wonders Kidogo.

Hatukatazwi Kuendeleza Mila, Ila Hatutakiwi Kuwanyima Watoto Haki Yao Ya Kimsingi Tena Kwa Madhara Yanayotokea Baada Ya Hizi Mila. Kwanini Tusisubili Baada Ya Elimu Ndio Ngoma Ifanyike?? Je Ngoma Ina Faida Economical Na Futuristic ya Mtoto?? K**a Jibu Yes Kwanini Tusiskip Hizi Shughuli Ili Watoto Wakishaenda Shule Waludipo Tuendelee Na Mila?? Kuna Wale Pia Anatumia Gharama Kubwa Kuita Shughuli Ikiisha Anakua Na Madeni Lukuki, Nani Kakuambia Ukimbilie Hii Kitu?? Inaumiza Sana Ila No Way Out. Tunaheshimu Mila Ila Mambo Yanayotokea Baada Ya Utekelezaji Wa Mila Ndo Zinafanya Tukosoe Utekelezaji Wake

NB : Picha Haihusiani na Andiko

Kikao Cha Baraza La Vijana Wilaya Ya Bagamoyo Likiendelea Katika Viwanja Vya Shule Ya Sekondari Kibindu Iliyopo Katika K...
30/12/2023

Kikao Cha Baraza La Vijana Wilaya Ya Bagamoyo Likiendelea Katika Viwanja Vya Shule Ya Sekondari Kibindu Iliyopo Katika Kata Ya Kibindu Wilaya Ya Bagamoyo.



MAGULUMATALI MABINGWA AZINUNI CUP Mashindano Ya AZINUNI Cup Yaliyokua Yanaendelea Katika Viwanja Vya Shule Ya Msingi Tal...
28/12/2023

MAGULUMATALI MABINGWA AZINUNI CUP

Mashindano Ya AZINUNI Cup Yaliyokua Yanaendelea Katika Viwanja Vya Shule Ya Msingi Talawanda Yametamatika Rasmi Leo Hii Na Timu Ya Magulumatali Kuibuka Mabingwa Wa Kombe Hilo.

Mindukene Ndio Walikua Wa Kwanza Kupata Goli Dakika Ya 5 Ya Mchezo Baada Ya Mchezaji Wao Amani Amani Kuifungia Timu Hiyo Bao Safi Akitumia Udhaifu Wa Mabeki Wa Magulumatili.

Dakika Ya 37 Ya Mchezo, Magulumatali Walisawazisha Bao Hilo Kupitia Kwa Beki Wao Rama Mtugani Baada Ya Kupiga Shuti Kali Lililomshinda Kipa Wa Mindukene, Kindoki.

Hadi Kipindi Cha Kwanza Kinaisha Timu Hizo Zikaenda Mapunziko Kwa Kutoshana Nguvu. Kipindi Cha Pili Timu Zote Mbili Zilifanya Mabadiliko Kwa Baadhi Ya Wachezaji, Mabadiliko Ambayo Hayakuzaa Matunda Na Hadi Dakika 90 Za Mchezo Huo Zinatamatika Timu Zote Zikatoshana Nguvu Ya Bao 1-1 Ndipo Mikwaju Ya Penati Ikapigwa na Magulumatali Kushinda Penati 3 Kwa 1.

Wakiongea Baada Ya Mchezo Huo, Manahodha Wa Timu Zote Mbili Wamefurahishwa Na Ubora Ulioneshwa Na Mpinzani Huku Nahodha Wa Mindukene, Aman Aman Akisema Kua Wao K**a Timu Watajipanga Kwa Michuano Ijayo Mana Hii Haikua Bahati Kwao. Pia Aliwapongeza Magulumatali Kwa Kushinda Kumbe Kwani Kwa Ubora Waliounesha Uwanjani Walistahili Ushindi , Huku Nahodha Wa Magulumatali Jose Alex Akisema Ushindi Walioupata Ni Ushindi Wa Wanamagulumatali Ambao Kwa Siku Za Karibuni Wamekosa Makombe Kadhaaa na Kutoa Tambo Kwa Wapinzani Kua Sasa Wamerudi Katika Ubora Wao, Pia Amefurshishwa Na Upinzani Uliooneshwa Na Mindukene Na Kukili Ya Kua Mechi Haikua Rahisi Kwa Ila Wanamshukuru Mungu Kwa Ushindi Huo.

Mashindano Hayo Yaliyoanza Kutimua Vumbi Rasmi Oktoba Mwaka Huu na Kuzikutanisha Timu 9 Kutoka Kata 3 Tofauti ,Leo Yametamatika Ambapo Bingwa Wa Michuano Hiyo Amejinyakulia Zawadi Ya Jezi Pea Moja Pamoja Na Mbuzi Wawili.

Address

65
Chalinze

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Magulumatali Yetu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category