08/01/2023
Ufuatao ni Mtiririko Wa Hatua Mbalimbali Zitakazo Muwezesha Mtu Yeyote Kufanya Upimaji Wa Eneo lake na kupata Hati Miliki Ya Ardhi,Kwa Maeneo Ya Upimaji Wa Kiwanja au shamba hapa Nchini Tanzania.
1.KUFANYA UKAGUZI WA ENEO HUSIKA.Hapa Ukaguzi unafanyika Ili kujua Eneo Hilo limepangwa Kwa Matumizi Gani kwenye Ramani ya Mipango Miji.Hapa Anatakiwa Kushirikishwa Surveyor kwa kuja site/Eneo ili kufanya utambuzi Kwa kuchukua Coordinate na kifaa cha kupimia (Handheld GPS) kwa Kuzunguka kwenye mipaka ya Eneo Husika.Baada Ya Hapo Surveyor Ataenda na Coordinate za Eneo husikq kwenye Halmashauri pamoja na wizarani ili kupata Majibu.
2.MATOKEO YA ZOEZI LA UKAGUZI-Eneo linaweza kukosa sifa au kuwa na sifa ya kupimika kulingana na Matokeo ya Ukaguzi uliofanywa,🔹Eneo linaweza kukosa sifa ya kupimika endapo Eneo Hilo litakua limeandaliwa Mchoro awali na kupangwa katika Matumizi ya kijamii Mfano Makaburi, Barabara,soko,,,nk🔹Eneo Husika kuwa na sifa ya kupimika K**a hakuna Mchoro au K**a Kuna Mchoro na Kuwa Katika Matumizi Ambayo Mtu Binafsi anaweza Kumiliki Mfano Makazi,hotel,biashara.
3.Uandaaji Wa Mchoro wa Viwanja ,Hapa Wataalam Wa Mipango Miji Wataandaa Mchoro wa Viwanja akionyesha mpangilio wa Viwanja vyenye ujazo wa Juu,kati na Chini (High,Medium and Low Density)Ikiwa ni Pamoja na Miundombinu Ya Usafirishaji Maeneo Ya wazi na soko au biashara.Baadae Utaandaliwa File kwa Ajili Ya kwenda Wizara likiambatanishwa na Ramani ya Mchoro wa Mipango Miji kwa Ajili ya kuidhinishwa rasmi kwa Upimaji wa Eneo Husika.
4.KIBALI CHA UPIMAJI-Hapa Mmiliki Halali Wa Eneo husika itabidi aandae Barua kwa Ajili ya kuomba kupimiwa eneo lake .Barua hiyo itapita serikali ya mtaa na Halmshauri husika.
5.UPIMAJI WA ENEO-Hapa Mtaalam wa Upimaji Ardhi (Surveyor) ataweka Mipaka Katika Eneo Husika kwa kutumia nondo(pin) au mawe (beacon) pia litaandaliwa file Kwa Ajili ya kwenda Wizarani likiambatanishwa na Ramani Ya Upimaji na Taarifa za muhusika/mmliki Wa Eneo.Na Mwishowe Ramani Hiyo hurudishwa Ikiwa imeidhinishwa na wizara ya Ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi.
6.Mmiliki Atakabidhiwa Ramani ya Upimaji Ambayo atapaswa kuitumia kuandaa Hati Miliki.
Ijue Ardhi Na Surveyor Obare #
0719-327463