05/06/2023
Imekuwa ni bandika bandua ya uuzaji wa viwanja pamoja na mashamba Kwa takribani Miaka minne (4).
Ni mafanikio ya aina yake kwangu binafsi na kampuni Kwa ujumla Kwa muda ambao nimetumikia kampuni ya cholemu investment ltd
Nitakuwa mchoyo wa fadhila k**a sitatoa shukrani zangu za dhati Kwa mkurugenzi wangu Kwa kunipa nafasi ambayo vijana wengi mitaani waliitamani
Namshukuru Kwa kunipa nafasi,kuniamini na kunivumilia mpaka na Mimi nakuwa miongoni mwa watu tegemezi ofisini
Hakika Kuna sehemu nimesogea kupitia cholemu,nimeongeza watu,nimeongeza uelewa,lakini hata kipato changu Cha Leo sio Cha jana
Mr mayunga kwangu Mimi ni k**a boss,ni k**a brother lakini ni k**a mtu wangu wa mfano (role model)
Nimejifunza mengi kutoka kwake,na pia namuombea Kwa mungu aendelee kumpa uhai mrefu ili sisi vijana tunaotamani kuwa wakubwa tuendelee kujifunza kupitia yeye🤲
Lakini pia sitakuwa mwema k**a sitamshukuru ndugu yangu Bruno victor (ujanjaardhi) Kwa kunishika mkono kutoka mtaani mpaka ofisini cholemu investment ltd,mungu akulipe brother 🤲unaishi katika moyo wangu.
Nawashukuru sana staff wenzangu Kwa ushirikiano mkubwa sana tangu naanza kazi🙏
Kwa muda wote huo yamekuja makampuni mengi sana ,wamekuja wafanyakazi wengi mnoo wenye uwezo mkubwa pengine kunizidi Mimi
Swali la kujiuliza;je Kila siku nitauza viwanja?,jamii itanifahamu Kwa kuwa muuza viwanja tu?jibu ni hapana.
Je Kila siku nitaendelea kuwa muajiriwa, jibu ni hapana,Taasi zinakuwa, zinahitaji watu wapya,zinahitaji ubunifu mpya zinahitaji radha mpya
Ipo siku nitaondoka cholemu 😭 aidha Kwa kutaka au kutokutaka ndio mfumo ulivyo,lakini natamani hiyo siku niondoke huku wote tukiwa na furaha
Waswahili wanasema ukitaka kutoka sehemu usitokee dilishani,fata utaratibu kumbuka kutokea ulipoingilia k**a ufanyavyo mwiba kwenye ngozi ya binadamu.
Sisi vijana maskini lazima Kwanza tutumwe,alafu tujitume, ndio na sisi tuwatume wengine ndio mfumo wetu.
Naombeni sapoti yenu k**a mlivyonisapoti kwenye viwanja
Twende tukasapoti Kwani Kuna vijana wenzetu wanapata rizki huku🙏🙏🙏
Ahsanteni🙏