Hustler Best Properties Co Ltd

Hustler Best Properties Co Ltd Tunauza Maeneo Ya Makazi,Biashara Na Uwekezaji Kwa Bei Nafuu

Hivi kusema "Boss Amefurahi" Kwa Kiluga Chenu Mnasemaje?🤩Dondosha Comment Yako👎☎ 0718 395 914📍Prime location📝100% free t...
10/06/2026

Hivi kusema "Boss Amefurahi" Kwa Kiluga Chenu Mnasemaje?🤩

Dondosha Comment Yako👎

☎ 0718 395 914
📍Prime location
📝100% free title deed.


10/06/2026

JUNIOR PLOT PACKAGE si package ya watoto pekee, bali ni zawadi ya usalama wa baadaye, mwanzo mzuri wa maisha na msingi wa mafanikio ya mtoto wako.

Tunafurahia kuona ikiendelea kuwa miongoni mwa package zinazopendwa zaidi na wazazi wenye maono ya mbali kwa ajili ya watoto wao.

Hivi unajua thamani halisi ya mtoto wako ipo kwenye elimu bora, malezi bora na uwekezaji wa mapema?

Unapomlea mtoto vizuri, ukamuwezesha kupata elimu na ukamjengea msingi wa uwekezaji kuanzia leo, unakuwa hujamuandalia tu maisha bora ya kesho, bali pia unachangia kujenga taifa lenye kizazi chenye maono, uwezo na uhuru wa kiuchumi.

Mpe mtoto wako thamani yake leo,achana na atajinunulia mwenyewe akikua...😊

, ndio mwanzo mwanzo mzuri wa kesho ya mtoto wako.

☎ 0718 395 914
📍Prime location
📝100% free title deed.


Furaha yetu ni kuona wateja wetu wakitimiza malengo yao ya uwekezaji kwa kumiliki viwanja vilivyopimwa na kuthibitishwa ...
09/06/2026

Furaha yetu ni kuona wateja wetu wakitimiza malengo yao ya uwekezaji kwa kumiliki viwanja vilivyopimwa na kuthibitishwa rasmi na Wizara ya Ardhi.

Hawa ni baadhi ya wawekezaji walioichagua miradi yetu ya na Kigamboni, na leo wanaendelea kutimiza ndoto zao za makazi bora na usalama wa uwekezaji wao.

Asanteni kwa kuichagua Hustler Best Properties, Hongereni kwa kuwa wawekezaji wa kweli.🙌

☎ 0718 395 914
📍Prime location
📝100% free title deed.





09/06/2026

Kuwa Wewe Katika Safari Ya Kumiliki Ardhi Yako.

Wengi wamejikuta wakichelewa kuanza kuwekeza kwenye ardhi kwa sababu ya kujifananisha na kutamani maisha ya wengine. Lakini ukweli ni kwamba, kila unayemwona leo akiwa hatua unayotamani kufikia, aliwahi kuanzia sehemu fulani akiwa na uwezo mdogo kuliko alionao sasa...

Uwekezaji wa ardhi haujengwi kwa kuiga lifestyle ya mtandaoni, bali kwa kufanya maamuzi sahihi kulingana na uwezo wako wa leo.

Kanuni ya uwekezaji ni ile ile: K**a huwezi kuamua, kuchagua na kuanza kwa bajeti ndogo, hata bajeti kubwa ikija haitabadilisha tabia hiyo. K**a unaona ugumu kulipia site visit leo, jiulize utawezaje kumiliki kiwanja kikubwa kesho bila kuanza hatua za leo?

Usisubiri uwezo mkubwa ndipo uanze. Anza na ulicho nacho, jifunze, tembelea miradi, fanya maamuzi, kisha endelea kukua hatua kwa hatua.

Maisha yanakuwa rahisi pale unapoamua kuwa wewe, kuishi ndani ya uwezo wako na kujenga ndoto zako kwa kasi yako mwenyewe.

Ardhi haimhitaji mkamilifu, inamhitaji mwenye maamuzi,Acha kujifananisha.

Kumbuka safari za site visit ni kila J Tano, J Mosi na J Pili,Fanya Booking mapema.

☎ 0718 395 914
📍Prime location
📝100% free title deed.



Kwako Wewe HUSTLER, Fanya Unachokipenda, Usipende Tu Unachokifanya.Ngoja nikusimulie story kidogo...Watu wengi wanadhani...
08/06/2026

Kwako Wewe HUSTLER, Fanya Unachokipenda, Usipende Tu Unachokifanya.

Ngoja nikusimulie story kidogo...

Watu wengi wanadhani kwamba nilisomea masuala ya upimaji wa ardhi (Land Survey) au Real Estate kwa taaluma. Ukweli ni kwamba mimi nimesomea Business Management.

Baada ya kumaliza masomo yangu, niliingia mtaani k**a vijana wengine wenye ndoto kubwa. Nikaanza kufanya biashara ndogo ndogo; nilifungua library za kukodisha CD, nikauza mkaa, nikafanya biashara ya vifaa vya simu (phone accessories) na biashara nyingine mbalimbali.

Lakini pamoja na biashara zote nilizokuwa nafanya, kulikuwa na jambo moja ambalo halikuwahi kutoka kichwani mwangu...

Ndoto ya kuwa mfanyabiashara mkubwa😄

Kwa wakati ule sikujua ni biashara gani ingenifikisha huko. Nilichojua ni kwamba siku moja nitakuwa mfanyabiashara mkubwa.

Kadri miaka ilivyopita, nikaanza kujikuta ninafurahia kuona watu wanapata makazi bora na kujiandalia maisha ya baadaye. Lakini swali ni je...

Nini hasa kilinisukuma kuingia kwenye biashara ya ardhi?

Ukweli ni huu...
Katika kipindi cha ukuaji wangu, niliondoka nyumbani mapema sana. Nikiwa Form Two nilianza kuishi Study Camp, na nilipofika Form Three nikaanza kupanga ghetto.

Nakumbuka wakati huo kodi yangu ya nyumba ilikuwa Tsh 8,000 kwa mwezi. Siku moja nikalipa kodi ya miezi sita mbele, jumla ya Tsh 48,000.

Lakini kilichonishangaza ni kwamba baada ya muda, bibi mwenye nyumba alikuja kunidai kodi wakati bado nilikuwa na miezi miwili mbele tayari nimeshalipia.

Tukio hilo liliniacha na maswali mengi sana...

Nikaanza kufikiria kwa undani kuhusu makazi, umiliki wa ardhi na changamoto ambazo watu wengi wanapitia kila siku.

Hapo ndipo safari yangu katika sekta ya ardhi ilipoanza.

Sikuwa na taaluma ya ardhi. Sikuwa mtaalamu wa upimaji. Nilianza k**a mwanafunzi wa maisha...mambo ya ku hustle hustle tu😄

Nilianza kujifunza kwa waliotangulia. Nilisikiliza, nilifuatilia, nilijifunza kwa vitendo na kwa makosa. Nilitumia takribani miaka miwili nikijifunza kazi hii mtaani kutoka kwa watu wenye uzoefu mkubwa.

Much respect kwa wote walionifundisha na kuniongoza...mungu awabariki sana 🙏, siku wakiridhia nitawataja hapa.

Itaendelea... Part 2.

08/06/2026

Happy Monday!
Wengi wamejikuta kwenye majuto baada ya kununua viwanja ambavyo havikuendana na malengo yao.

Kumbuka, suala si kununua kiwanja tu, bali kununua kiwanja kinachoendana na matumizi na ndoto zako za baadaye.

Kununua kiwanja si kosa. Kosa ni kufanya maamuzi bila kuwa na elimu sahihi kuhusu vipimo na makundi rasmi ya viwanja.

Je, unajua kuwa kwa mujibu wa miongozo ya upangaji wa matumizi ya ardhi nchini, viwanja hugawanywa katika makundi makuu matatu?

✅ Low Density–Viwanja vikubwa kwa makazi yenye msongamano mdogo.

✅ Medium Density–Viwanja vya ukubwa wa kati kwa makazi ya kawaida.

✅ High Density–Viwanja vidogo kwa maeneo yenye msongamano mkubwa wa watu.

Kabla hujanunua kiwanja, hakikisha unafahamu ukubwa wake, matumizi yake na k**a kinaendana na malengo yako ya uwekezaji.

Elimu kwanza, maamuzi baadaye....Dua/Sala yetu ni ile ile Tunakuombea Jina lako liandikwe kwenye hati ya kiwanja chako katika miradi yetu iliyopo Kigamboni na Bagamoyo Makurunge.

📍STAR CITY-KIGAMBONI CHEKA
Tsh 24,000/= Cash
Tsh 26,000/= Awamu Miezi sita 6
Anza Na 3M.

📍TANZANITE CITY-MBUTU MKWAJUNI
Tsh 25,000/= Cash
Tsh 27,000/= Awamu miezi sita 6
Anza na 3M.

📍BAGAMOYO MAKURUNGE
Tsh 10,000/= cash
Tsh 12,000/= awamu miezi sita 6.
Anza na 50%.

☎ 0718 395 914
📍Prime location
📝100% free title deed.





KIWANJA CHAKO KINAKUSUBIRI...! Site Visit Si Safari Tu Ya Kuja Kuona Kiwanja, Bali Ni Safari Ya Kupata Majibu Ya Maswali...
05/06/2026

KIWANJA CHAKO KINAKUSUBIRI...!

Site Visit Si Safari Tu Ya Kuja Kuona Kiwanja, Bali Ni Safari Ya Kupata Majibu Ya Maswali Yako, Kujifunza Kuhusu Uwekezaji Wa Ardhi Na Kuona Ushuhuda Wa Kweli Kwa Walioanza Kuchukua Hatua.

Site Visit Ndiyo Mwanzo Wa Future Yako, Twwnzetu Site Weekend Hii...!

Site Visit Fee: Tsh 20,000/= Only.

☎ 0718 395 914
📍Prime location
📝100% free title deed.





05/06/2026

Moja Ya Maswali Tunayoulizwa Kila Siku Na Wateja Wapya Ni:

📍"Mradi Upo Umbali Gani Kutoka Ferry Au Daraja la Nyerere?"

✅ Kutoka Ferry hadi Star City–Km24 (takribani dakika 51)
✅ Kutoka Daraja la Nyerere hadi Star City–Km28 (takribani dakika 58)

Kumbuka, thamani ya ardhi haipimwi kwa umbali wake kutoka katikati ya jiji pekee, bali kwa kasi ya maendeleo ya eneo, miundombinu iliyopo na uwezo wake wa kuongezeka thamani hapo baadaye.

Maeneo mengi yaliyokuwa yakionekana mbali miaka michache iliyopita leo ndiyo maeneo yanayotafutwa zaidi na wawekezaji wenye maono.

ipo katika eneo lenye ukuaji mkubwa Kigamboni, mahali ambapo una nafasi ya kununua leo kwa gharama nafuu kuliko utakavyonunua kesho.

Usisubiri Vimeisha ndipo uanze kutafuta kiwanja. Wekeza mapema, linda fedha zako, na urithi wa familia yako.

Karibu Kigamboni, mahali sahihi pa kujenga kesho yako.

☎ 0718 395 914
📍 Prime location
📝 100% free title deed.





03/06/2026

Hawa Ni Sehemu Ya Majirani Waliokaribu Sana Na Mradi Pendwa Uliopo Kigamboni Cheka, Yaani Wapo Opposite Na Mradi.

Tafadhali Usituulize Tena Kuhusu Umeme, Barabara, Maji Wala Majirani...😄

Njoo Ujenge Uhamie.

☎ O718 395 914
📍 Prime Location
📝100% Free Title Deed.

Address

Chamazi Complex Mkabala Na Azam Stadium
Dar Es Salaam
15116

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hustler Best Properties Co Ltd posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Hustler Best Properties Co Ltd:

Share

Category