08/06/2026
Kwako Wewe HUSTLER, Fanya Unachokipenda, Usipende Tu Unachokifanya.
Ngoja nikusimulie story kidogo...
Watu wengi wanadhani kwamba nilisomea masuala ya upimaji wa ardhi (Land Survey) au Real Estate kwa taaluma. Ukweli ni kwamba mimi nimesomea Business Management.
Baada ya kumaliza masomo yangu, niliingia mtaani k**a vijana wengine wenye ndoto kubwa. Nikaanza kufanya biashara ndogo ndogo; nilifungua library za kukodisha CD, nikauza mkaa, nikafanya biashara ya vifaa vya simu (phone accessories) na biashara nyingine mbalimbali.
Lakini pamoja na biashara zote nilizokuwa nafanya, kulikuwa na jambo moja ambalo halikuwahi kutoka kichwani mwangu...
Ndoto ya kuwa mfanyabiashara mkubwa😄
Kwa wakati ule sikujua ni biashara gani ingenifikisha huko. Nilichojua ni kwamba siku moja nitakuwa mfanyabiashara mkubwa.
Kadri miaka ilivyopita, nikaanza kujikuta ninafurahia kuona watu wanapata makazi bora na kujiandalia maisha ya baadaye. Lakini swali ni je...
Nini hasa kilinisukuma kuingia kwenye biashara ya ardhi?
Ukweli ni huu...
Katika kipindi cha ukuaji wangu, niliondoka nyumbani mapema sana. Nikiwa Form Two nilianza kuishi Study Camp, na nilipofika Form Three nikaanza kupanga ghetto.
Nakumbuka wakati huo kodi yangu ya nyumba ilikuwa Tsh 8,000 kwa mwezi. Siku moja nikalipa kodi ya miezi sita mbele, jumla ya Tsh 48,000.
Lakini kilichonishangaza ni kwamba baada ya muda, bibi mwenye nyumba alikuja kunidai kodi wakati bado nilikuwa na miezi miwili mbele tayari nimeshalipia.
Tukio hilo liliniacha na maswali mengi sana...
Nikaanza kufikiria kwa undani kuhusu makazi, umiliki wa ardhi na changamoto ambazo watu wengi wanapitia kila siku.
Hapo ndipo safari yangu katika sekta ya ardhi ilipoanza.
Sikuwa na taaluma ya ardhi. Sikuwa mtaalamu wa upimaji. Nilianza k**a mwanafunzi wa maisha...mambo ya ku hustle hustle tu😄
Nilianza kujifunza kwa waliotangulia. Nilisikiliza, nilifuatilia, nilijifunza kwa vitendo na kwa makosa. Nilitumia takribani miaka miwili nikijifunza kazi hii mtaani kutoka kwa watu wenye uzoefu mkubwa.
Much respect kwa wote walionifundisha na kuniongoza...mungu awabariki sana 🙏, siku wakiridhia nitawataja hapa.
Itaendelea... Part 2.