Fadhila na afya yako

Fadhila na afya yako Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Fadhila na afya yako, Real Estate, kimara, Dar es Salaam.

🛑 *UJUE UGONJWA WA P.I.D*Maambukizi katika mfumo wa uzazi wa mwanamke kwa kitaalamu Pelvic Inflamatory Diseases au kwa k...
31/07/2021

🛑 *UJUE UGONJWA WA P.I.D*

Maambukizi katika mfumo wa uzazi wa mwanamke kwa kitaalamu Pelvic Inflamatory Diseases au kwa kifupi PID, ni moja ya matatizo ambayo huwaathiri sana wanawake. Kwa kawaida maambukizi haya huusisha shingo ya uzazi (cervix) hali ambayo hujulikana k**a cervicitis, nyama ya mfuko wa uzazi (endometrium) ambayo kitaalamu huitwa endometritis, na mirija ya uzazi (fallopian tubes) hali ijulikanayo kitabibu k**a salpingitis.

*_PID husababishwa na nini?_*

Pamoja na aina kadhaa za vimelea kuhusishwa na PID, vimelea vya jamii ya Neisseria Gonorrhoeae pamoja na Chlamydia trachomatis ndivyo vinavyoongoza kwa umaarufu zaidi katika kusababisha PID kwa akina mama.

*Je mwanamke huambukizwaje PID?*

Kuna njia kadhaa ambazo mwanamke anaweza kuambukizwa PID. Njia hizo ni pamoja na

✅Kufanya ngono isiyo salama.

✅Maambukizi ya njia ya uzazi hasa kipindi mara baada ya kujifungua (au postpartum period)

✅Maambukizi ya njia ya uzazi mara baada ya kutoa mimba kwa njia zisizo salama (post abortion) au mara baada ya mimba kutoka (miscarriage)

✅Kutumia vipandikizi vya ndani ya mfuko wa uzazi (IUCD) k**a njia mojawapo ya uzazi wa mpango.

✅Kuambukizwa kupitia damu iliyo na vimelea vya PID.

*Dalili za PID ni zipi?*

Zipo dalili kadhaa za ugonjwa huu wa PID. Miongoni mwa dalili hizi ni :-

✅Mwanamke kuhisi maumivu ya tumbo hasa maeneo ya chini ya kitovu

✅Kupata maumivu ya mgongo.

✅Mwanamke kupata utoko mchafu sehemu za siri. Utoko huu huambatana na harufu mbaya.

✅Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa.

✅Kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa.

✅Kutoka damu bila mpangilio wakati wa hedhi.

✅Kupata homa.

✅Wakati fulani kuhisi kichefuchefu na
Pia kutapika.

⏩Ugonjwa huu wa Pelvic Inflammatory Diseases *P.I.D* unakuwa kwa Kasi kubwa na baadhi ya wanawake hupata madhara makubwa baadae hususani Ugumba kutokana na kupuuzia matibabu. Ikiwa unaona dalili tajwa hapo juu jitahidi kuanza matibabu taratibu kabla haujapata madhara ambayo yanaweza kugharimu Maisha yako kwa ujumla.
✍🏿✍🏿✍🏿✍🏿✍🏿✍🏿✍🏿✍🏿
*MUWE NA MCHANA ULIO MWEMA NYOTE, JIKINGE NA P.I.D epuka UGUMBA*

*FAHAMU HIZI SABABU KUMI(10) ZINAZOWEZA KUPELEKEA UJAUZITO KUHARIBIKA.* ✍️kuna sababu nyingi zinazoweza sababisha mimba ...
15/07/2021

*FAHAMU HIZI SABABU KUMI(10) ZINAZOWEZA KUPELEKEA UJAUZITO KUHARIBIKA.*
✍️kuna sababu nyingi zinazoweza sababisha mimba kutoka lakini leo nteanda kongelea zile muhimu ili kila mtu k**a iko ndani ya uwezo wake aweze kuzuia pale anpopata mimba.
✍️matatizo ya vimelea vya urithi: kawaida mbegu za mwanaume huchangia pea 23 za vimelea vya urithi yaani chromosomes na yai la k**e hichangia vimelea 23 pia kwa ajili ya mtoto atakayezaliwa, lakini kwenye hali isiyo ya kawaida namba hiyo ikiongezeka au kushuka husababisha mimba kutoka ndani ya muda mfupi.
✍️magonjwa; kuna magonjwa mengi endapo hayatatbiwa wa muda muafaka husababisha mimba kutoka muda wowote ule yaani inaweza kua mwanzoni au mwishoni.mfano. malaria, kisukari, pressure, kaswende, virusi vya ukimwi, U.T.I, toxplasmosis,rubella, na herpes simplex virus.
✍️matatizo ya kizazi; kuna magonjwa mengi yanayoathiri kizazi moja kwa moja na huweza kuleta kutoa mimba kirahisi sana mfano wa magonjwa hayo ni uvimbe wa ndani ya kizazi,ulegevu wa mlango wa uzazi na kadhalika.
✍️matumizi ya dawa; ukiwa mjamzito hutakiwi kutumia dawa yeyote bila kuandikiwa na daktari, kuna dawa nyingi sana zinaweza kutoa mimba mfano fragile, albendazole,misoprostol, dawa ya mseto ya malaria, doxycline, na nyingine nyingi.
✍️utapiamlo; mwanamke mwenye upungufu wa madini muhimu mwilini k**a calcium, potassium na sodium lakini pia wanga, protini, vitamini na kadhalika. upungufu huu humfanya mwanamke ashindwe kubebeba mimba mpaka kujifungua na hata akijifungua huweza kuzaa mtoto mwenye mapungufu fulani ya kiakili.
✍️matatizo ya homoni; mwanamke ana kiwango maalumu cha homoni za uzazi ambacho anatakiwa awe nacho ili mimba iweze kutungwa na kukua. kiwango hiki kikiwa juu sana au chini sana husababisha mimba kuharibika.
✍️Aina ya maisha ya mjamzito; matumizi ya pombe na sigara kipindi cha ujauzito ni hatari sana kwani huingilia mfumo wa homoni na uzazi na kusababisha mimba kuharibika.
✍️umri mkubwa; kubebe mimba kwenye umri mkubwa huchangia sana mimba kuharibika kwani kipindi hiki viungo vya uzazi na mfumo wa homoni unakua umepungua nguvu sana hivyo mimba.

Address

Kimara
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Fadhila na afya yako posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category