02/08/2022
ELIMIKA NA WAZALENDO PROPERTIES!!!!
HIZI NDIO HATUA MUHIMU ZA KUFUATA UNAPOHITAJI KUNUNUA KIWANJA
1. Mjue mmiliki halali wa eneo kwa muda huo.
Kumekua na tabia ya watu wengi kukutana na madalali na kuishia kufanya nao mauziano bila ya mmiliki kuwepo/kuwa na taarifa. Hii imepelekea watu wengi kutapeliwa ama kuuziwa kiwanja kwa bei isiyo sahihi.
Kuweza kumjua mmiliki, jitahidi kuzungumza na majirani wa eneo hilo kabla ya kufanya maamuzi ya kununua. Sisitiza kuonyeshwa ofisi au makazi yake ili kukitokea tatizo ujue pa kumpata.
2. Usifanye malipo siku ya kwanza baada ya kuona kiwanja.
Haijalishi ardhi uliyooneshwa imekuvutia kwa kiasi gani, tafuta muda wako urudi katika eneo husika bila muuzaji na uulize kwa majirani au wazawa ili kupajua vizuri. Hii itakusaidia kuhakiki taarifa za muuzaji k**a ni za kweli na eneo halijauzwa kwa mtu mwingine.
3. Ijue historia ya eneo husika
Baadhi ya ardhi zimekua kwenye migogoro baina ya wananchi na serikali au familia.
Fanya uchunguzi wa kina juu ya historia ya ardhi unayotaka kununua kupitia majirani na ofisi za serikali ya mtaa/kijiji.
Hii itakurahisihia kujua eneo na utamaduni wa watu wa eneo hilo hivyo kufanya maamuzi sahihi ya kununua au kuacha.
4. Kuwa mtu wa kudadisi kwa kuuliza maswali
Usikubali kupelekwa site na muuzaji akawa ndie mzungumzaji pekee bila wewe kuuliza maswali.
Kupitia maswali utapata kumfahamu vizuri mmiliki, je eneo hilo amerithi au amenunua?
Ana nyaraka halali za umiliki? Ni kampuni au mtu binafsi?
Ikibidi akuoneshe hati miliki kuthibitisha yeye ndie mmiliki.
5. Upatikanaji wa huduma za kijamii
Wauzaji wengi wana tabia ya kusema kuwa huduma za kijamii zipo karibu, kiuhalisia zinakua zipo mbali au hakuna kabisa.
Tumia muda wako kuhakikisha ikibidi akuoneshe mahali zilipofika.
Huduma muhimu kwa eneo la makazi ni maji, umeme, shule, hospitali na barabara inayofikika muda wote.
6. Ufanyaji wa malipo
Hiki ni kipengele muhimu sana. Malipo ni vizuri yakifanyika kwa njia za kielektroniki (benki, mitandao ya simu) na ikilazimu kutoa cash akupatie risiti ya uthibitisho. Ukimaliza malipo ni wajibu wa muuzaji kukupatia Hati miliki halali inayotambulika na serikali.
Baada ya hayo yote utakua umejipatia ardhi yako kihalali na salama.
ndio rasilimali pekee isiyoshuka thamani.
KWA VIWANJA BORA VISIVYO NA MIGOGORO TUPIGIE: 0629705684 (Watsapp) / 0684074721