17/12/2022
MAMBO YA MUHIMU YA KUZINGATIA KABLA HUJANUNUA ARDHI AU NYUMBA (ili ununue ardhi salama)
1⃣. Mshirikishe mpima ardhi (land surveyor), mpima ardhi anahitajika ili aweze kukufanyia ukaguzi wa eneo lako ili kutambua eneo husika limepangiwa kwa ajili ya matumizi gani katika ramani ya mipango miji (ambayo ni ramani inayoonyesha matumizi mbalimbali ya katika ardhi mf barabara, makazi,eneo la wazi n.k)
2⃣. Shirikisha majiran wa eneo unalotaka kununua, ili uweze kutambua muuzaji wa eneo ni halali au sio, na pia itakusaidia kujua k**a eneo halina migogoro. (Fanya mahojiano na majiran bila muuzaji kujua)
3⃣. Hakiki umiliki wa eneo husika serikali ya mtaa au k**a kiwanja kimepimwa basi unaweza kupata taarifa zake halmashauri husika.
4⃣. Tengenezeza mikataba ya mauziano ya ardhi (sale agreement) ambayo huandaliwas na mwanasheria
5⃣. Kamilisha malipo kwa njia sahihi ya kibenki