Jipe Moyo

Jipe Moyo Lengo ni Kukutia Moyo ili Ujue Ushindi Upo na Hayo Maisha Yatapita Tu

24/12/2025

Maana Bwana Yesu Amesikia Sauti ya Kilio Chako.

Hajiri Mamaye na Ishimaili yaani Aliyekuwa Mfanyakazi wa Ndani wa Ibrahimu...Kuna majira alipotia wakati mgumu..

Alipolazimika kuondoka mikono i mwa Mwajiri wake...Alifika Mahali pq Jangwa, na Maji Yakawa Yameisha....Alikata Tamaa na Kuiona Mauti Kwake na Kwa Mwana Wake...

Ndipo Malaika wa Mungu alipotokea na kumwambia ASIOGOPE kwa maana Mungu Amesikia Kilio Chake (mtoto)...

Nami k**a Mqlaika wa Bwana Ninakutia Moyo Majira haya ya Kwamba Usiogope kwa maana Bwana Amesikia Kilio cha Sala Zako...Hizi Ndizo Habari Nilizopewa na Bwana Nikupe...Sema; Ameni.

*Tazama* : Mwanzo 21:15 Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja.

16 Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, akapaza sauti yake, akalia.

17 Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko.

Kwa Jumbe Zaidi za Faraja na Matumaini Tafadhali Tembelea na uFollow Channel Yetu

( *Bonyeza Linki* )

Follow the Jipe Moyo 🫀❤️ Utashinda 💪💪🤝 channel on WhatsApp: https://whatsapp.com/channel/0029Vb7ZJLR9hXFGDfQuxT2D

  Maana Bwana Yesu Amesikia Sauti ya Kilio Chako.Hajiri Mamaye na Ishimaili yaani Aliyekuwa Mfanyakazi wa Ndani wa Ibrah...
24/12/2025

Maana Bwana Yesu Amesikia Sauti ya Kilio Chako.

Hajiri Mamaye na Ishimaili yaani Aliyekuwa Mfanyakazi wa Ndani wa Ibrahimu...Kuna majira alipotia wakati mgumu..

Alipolazimika kuondoka mikono i mwa Mwajiri wake...Alifika Mahali pq Jangwa, na Maji Yakawa Yameisha....Alikata Tamaa na Kuiona Mauti Kwake na Kwa Mwana Wake...

Ndipo Malaika wa Mungu alipotokea na kumwambia ASIOGOPE kwa maana Mungu Amesikia Kilio Chake (mtoto)...

Nami k**a Mqlaika wa Bwana Ninakutia Moyo Majira haya ya Kwamba Usiogope kwa maana Bwana Amesikia Kilio cha Sala Zako...Hizi Ndizo Habari Nilizopewa na Bwana Nikupe...Sema; Ameni.

*Tazama* : Mwanzo 21:15 Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja.

16 Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, akapaza sauti yake, akalia.

17 Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko.

Kwa Jumbe Zaidi za Faraja na Matumaini Tafadhali Tembelea na uFollow Channel Yetu

( Bonyeza Linki )

Follow the Jipe Moyo 🫀❤️ Utashinda 💪💪🤝 channel on WhatsApp: https://whatsapp.com/channel/0029Vb7ZJLR9hXFGDfQuxT2D

Follow Jipe Moyo 🫀❤️ Utashinda 💪💪🤝's WhatsApp channel. Join 37 followers for the latest updates.

05/11/2024

Keep This: Kukosoana ni Afya...Kuvumiliana Ni Ukomavu

Wimbi Kubwa  Linalosukasuka Uongozi Kwa Sasa, Ni Viongozi Kulinda Kiti; Kuliko Kusudi la Wao Kuwepo Hapo. Hawajui Kiti n...
05/11/2024

Wimbi Kubwa Linalosukasuka Uongozi Kwa Sasa, Ni Viongozi Kulinda Kiti; Kuliko Kusudi la Wao Kuwepo Hapo.

Hawajui Kiti ni Kwa Ajili ya Kusudi, Na Kusudi ni Kwa Ajili ya Maono.

Nidhamu ya Uwoga, Inalinda Mkate; Ujasiri Unalinda Kusudi.

Maisha ya Wokovu: Kuna Wakati Hata K**a Huoni mbele; Muamini Aliyekutangulia, yaani Kristo. Kwa hiyo usitumie Nguvu Nyin...
02/11/2024

Maisha ya Wokovu: Kuna Wakati Hata K**a Huoni mbele; Muamini Aliyekutangulia, yaani Kristo. Kwa hiyo usitumie Nguvu Nyingi Sana Kutazama Mbele, Bali Tazama Alipokanyaga ili Na Wewe Ukanyage.

By Mwalimu Oscar Samba

   Mic Za Kuvaa KichwaniLaki Moja na 20 Ikiwa Moja; _Ikiwa ni Ofa ya Badala ya Laki na 80_ .Na Mbili ni Laki na Nusu.074...
27/10/2024

Mic Za Kuvaa Kichwani
Laki Moja na 20 Ikiwa Moja; _Ikiwa ni Ofa ya Badala ya Laki na 80_ .
Na Mbili ni Laki na Nusu.
0742942772, _Tuna Tuma Popote Nchini._ Afya ya Muhubiri, Boresha Huduma Yako*

  Mic Za Kuvaa Kichwani* Laki Moja na 20 Ikiwa Moja; _Ikiwa ni Ofa ya Badala ya Laki na 80_ .Na Mbili ni Laki na Nusu.07...
19/10/2024

Mic Za Kuvaa Kichwani*
Laki Moja na 20 Ikiwa Moja; _Ikiwa ni Ofa ya Badala ya Laki na 80_ .
Na Mbili ni Laki na Nusu.
0742942772, _Tuna Tuma Popote Nchini._

Linda Afya ya Muhubiri, Boresha Huduma Yako

Nimeyaandika haya kwenye kitabu cha Uamsho Ninachokiandika hivi Sasa...Wala usijaribu kufikiri kuomba au kumuomba Mungu ...
18/10/2024

Nimeyaandika haya kwenye kitabu cha Uamsho Ninachokiandika hivi Sasa...

Wala usijaribu kufikiri kuomba au kumuomba Mungu akuondole mambo magumu katika picha ya kuishi maisha tambarare k**a njia ya kukuwezesha kutenda vyema bila kukata tamaa. La muhimu ni wewe kujikita zaidi katika kumuomba Mungu akuwezeshe, kuwa na uwezo wa kustaimili mambo magumu na sio kukimbilia kutaka yaondoke yote au kabisa. Ni lazima kutambua ya kuwa kazi ya Mungu ni vita, na k**a ni vita lazima sisi tuwe askari wenye uwezo, mbinu stahiki; sanjari na vifaa hitajika. Na viatu vya utayari ni silaha muhimu sana.

Vita ya kiroho bila utayari wa vita, ni sawa na kujaribu kuandaa shindano la mbio ndefu, alafu wanariadha ni vipofu. Watakwama tu kutokana na sifa ya aina hii ya mashindano. Sio kwamba sio wanariadha, ila tatizo ni kupoteza uwezo wa kuona.

By Mwl Oscar Samba 0759859287

Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha IMANI SAHIHI, Katika Mada ya Misingi na Tabia za Imani Sahihi.katika mada hii ya ...
18/10/2024

Ni Sehemu ya Kitabu Chetu Tarajiwa cha IMANI SAHIHI, Katika Mada ya Misingi na Tabia za Imani Sahihi.

katika mada hii ya kwanza, na kisha Misingi.

Mwalimu Oscar:
Mwl OSCAR SAMBA ( )
:
Lengo la kitabu hiki ni kukuwezesha kuijua au kuitambua imani ya kweli, na kuzifahamu hila za adui Shetani katika imani potofu; ikiwemo namna ya kuzitofautisha na ile ya kweli na jinsi ya kuzishinda.

Misingi na Tabia za Imani Sahihi
Maana ya Imani. Katika Biblia na hata maisha yetu ya kawaida, neno imani limegawanyika katika maana zaidi ya moja, na huweza kuwa na maana kuu mbili. Mosi ni ile imani k**a kuwa na hakika ya jambo unalolitarajia ambalo bado hujalipata ama kuliona ila unamatumaini nalo. Waebrania 11:1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.

Unganisha na hili andiko; Warumi 8:24 Kwa maana tuliokolewa kwa taraja; lakini kitu kilichotarajiwa kikionekana, hakuna taraja tena. Kwa maana ni nani anayekitarajia kile akionacho?

Maana ya Pili ya Neno Imani: Ni mfumo au "settings" ya mambo muhimu yenye kunuia kuunda aina fulani ya njia ya mtu; kimtazamo, fikra na hatimaye kimatendo, (kiimani "faith:") yenye kufuma namna ya kuabudu kwake, kusali, miiko fulani na maadili muhimu ya kuishi hapa ulimwenguni; sanjari na nini kitatokea k**a miiko au maadili hayo yatavunjwa au kuheshimiwa: yaani adhabu na dhawabu kwa maisha ya sasa na baada ya kifo. (Imani nyingi zina hatima fulani au maisha fulani baaada ya kifo, ambayo hutokana na jinsi muhusika alivyoishi humu ulimwenguni.)
Kwa ujumla imani au "belief" tuna weza kuiita ni dini. Neno dini kiswahili ni neno la Kiarabu lenye maana ya njia. Kwa hiyo ni njia inayosadikika (neno kusadikika limewekwa ili kujumuisha imani mbalimbali) kumuamini Mwenyezi Mungu, pamoja na kutembea katika njia zake.

Mfano wa imani au dini hizi ni Uislamu, dini zenye kuabudu mizimu au zile za asili kwa baadhi ya jamii, Ukristo katika Wokovu (Wapentekoste), Ukristo katika Romani Catholic, Ukristo katika Usabato, Ukristo katika Lutheran, Ukristo katika Anglikana, na Ukristo katika madhehebu mbalimbali. Pia kumeibuka kundi jingine ambalo leo hii baadhi ya Wanatheolojia huliita "New Pentecostal Group." Yaani kundi jipya la kipentekoste. Hawa ndio wale ambao wamekuja na mifumo mipya ya ibada ikiwemo matumizi ya chumvi, maji, mafuta, na kadhalika. Japo nami binafsi jina hilo sikubaliani nalo maana hatuna upentekoste mpya, kwani k**a kuna mpya basi wazamani u wapi?
Nakundi hili halikubali kuwa wa zamani maana hao ndio halisi. Labla liitwe chipukizi jipya la kipentekoste.
Hapo juu nilipoorodhesha hizo dini, hususani katika eneo la Kikristo, k**a dhehebu lako halijatajwa usikwazike, na utajaji huo ni kwa mujibu wa uchambuzi wangu. Japo ndio ulio sahihi, maana huwezi kuutaja Ukristo k**a dini kwa sura ya kutaka madhehebu yote yanayotumia Biblia yawe ni njia moja la! Maana humo ndani kiuhalisia njia zao zinatofautiana sana. Wapo wanaokubaliana na kufanana kwa sehemu, hao huweza kukaa kundi moja. Lakini la muhimu la kufahamu ni kwamba Yesu hakuanzisha dini bali alianzisha Ukristo. Na mkristo siye yule wenye jina la Kikristo kwa jinsi ya mwilini au kujulikana kwake, wala anayeshiriki ibada katika kanisa linalojulikana linatumia Biblia, bali ni yule ambaye anamuamini YESU Kristo na kuyaishi maisha yake. Yaani ni mfuasi wa Kristo Yesu. Hapa wokovu haukwepeki.

Maana ya Misingi
Msingi maana yake ni mambo muhimu au vitu muhimu vinavyotoa sababu ya uwepo wa kitu, au vinavyoshikilia maisha ya kitu ama vinavyobeba uimara au uwepo wake. Nyumba ya nguzo nne ukiondoa moja ni umedhuru uimara wa uwepo wake. Nyumba ukigusa msingi wake kwa kudhuru mawe ya msingi ni umetishia uhai au uimara wake.

Taasisi yenye malengo matano, ukigusa moja ni umedhuru sababu za uanzishwaji wake. Kiini cha uwepo wake.
Alikadhalika katika imani yoyote ile kuna mambo muhimu yanayotoa sababu za udhabiti wake. Kwenye Ukristo ule halisia ulioasisiwa na Yesu Kristo kuna mambo muhimu yanayoitwa msingi. Ni misingi ya imani hii ya wokovu.

Mfano katika Uislamu kuna nguzo kuu 5, hizo huufanya Uislamu uwe Uislamu. Ikiwemo zaka, kuhiji Maka, Mfungo kipindi cha mwezi Ramadhani na kadhalika. Kwetu Wokovu, Ubatizo, Uungu wa Yesu Kristo, Biblia kuwa ni Neno la Mungu, Yesu ni Mwana wa Mungu, Kujazwa Roho Mtakatifu ni miongoni mwa Misingi muhimu.
Nasi kuna mambo muhimu ukiyaona unafahamu fika hii ni imani sahihi ya Kipentekoste au wokovu. Ndiyo imani ambayo Biblia inamaanisha inapofika swala la kumuabudu Mungu katika Roho na Kweli.

Tafadhaali funga mkanda sasa maana k**a ni ndege inakaribia kuanza kupaa, kqmq ni "Bus" basi safari ndo inaanza. Tunaanza sasa uchqmbuzi wa kitabu chetu, tuanze na Imani katika mada hii ya kwanza, na kisha Misingi.
1. Imani Katika Utatu Mtakatifu
2.
3.

Dalili na Tabia, au Viashiria vya Imani Potofu
Namna ya Kujiepusha na Imani Potofu
Ombea Macho Yako ya Ndani....yatiwe nuru.

Kitabu kikitoka Kitafute..

http://www.ukombozigospel.blogspot.com
Tumeunda Channel ya WhatApp, Tufolo; https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h
Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD
Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk
Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/
Kwa Maombi +255759859287
Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook: https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbWKwL

Nikutakie Siku Njema

mafundisho ya neno la Mungu, Mahubiri mwalimu mchungaji Yesu Roho Mtakatifu maombi madhabahu malaika biblia injili nyimbo upako mtume nabii Oscar

Tatizo Kubwa la Viongozi wa Kiafrika Sio Kukosa Maono; Ni Kushindwa Kupandikiza Maono Kwa Watu Wanaowaongoza. Hawajui Ha...
18/10/2024

Tatizo Kubwa la Viongozi wa Kiafrika Sio Kukosa Maono; Ni Kushindwa Kupandikiza Maono Kwa Watu Wanaowaongoza. Hawajui Hakuna Mkuu wa Jeshi Anayeshinda Vita Kutokana na Uwezo Wake Binafsi tu; Bali ni Kwa Sababu Amefanikiwa Kuandaa Jeshi Zuri. Ubora wa Kocha Unapimwa Kutokana na Uwezo Wake wa Kuandaa Timu Nzuri.
Ukifeli Kuwafanya Wafikiri K**a Wewe, Uwe na Hakika Watafikiri K**a Wao; Na Watatenda Kiholela.

By Mwalimu Oscar Samba

Address

Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jipe Moyo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category